TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Monday, September 30, 2013

HII NDIYO SHERIA BWANA.ALIYETUHUMIWA KUMTEKA NA KUMTESA DR ULIMBOKA AHUKUMUIWA JELA MWEZI MMOJA AU KULIPA FAINI YA ELFU KUMI!

Joshua Mulundi (21) raia wa Kenya aliyekuwa anatuhumiwa kumteka na kumtesa Dk Ulimboka na baadaye kuachiwa huru na mahakama na baadaye kufunguliwa kesi ya kulidanganya jeshi la polisi, ahukumiwa kifungo cha mwezi mmoja jela ama kulipa fine ya shilingi elfu moja (1000) baada ya kukiri kosa lake. 

Hata hivyo mshtakiwa huyo alifanikiwa kulipa faini hiyo na hivyo kuachiwa huru baada ya mmoja wa waandishi wa habari kumopatia hiyo pesa

ASKARI WA ZIMA MOTO WACHARUKA, WAMPA ADHABU KALI KIJANA ALIYEPIGA SIMU NA KUWADANGANYA NYUMBA INAUNGUA!




Mmoja wa wakazi wa Rugelele kata Rujewa wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya  DUKA MKWILA[20]ni miongoni mwa wananchi waliopiga simu za uongo katika kikosi cha zimamoto mkoa wa mbeya akiwa amepewa adahabu ya kuosha gari la zimomoto

Hata hivyo DUKA alikiri kutenda kosa na kuomba msamaha kwa jeshi hilo ambapo aliachiwa huru na kisha kurejea kwao huku akijutia kosa alilolifanya na kuahidi kutorudia tena.





JESHI la zimamoto na uokoaji limewataka wananchi kuacha matumizi mabaya ya miito ya simu ya dharula kwa Jeshi hilo ili kuepusha usumbufu kwa Jeshi pindi wanapopigiwa simu za dharula.

Wito huo umetolewa na Jeshi hilo baada ya kupata kero za mara kwa mara kutoka kwa wananchi wanaopiga simu kwenye Jeshi hilo wakihitaji huduma za gari hilo lakini wanapofika eneo waliloelekezwa wanakuta hakuna tukio lolote.
Wamekuwa wakipokea simu nyingi za uongo hivyo serikali kuingia gharama kubwa za mafuta ambayo yangetumika kwenye maafa pindi yanapotokea.

Mmoja wa wakazi wa Rugelele kata Rujewa wilaya ya MBARALI DUKA MKWILA[20]ni miongoni mwa wananchi waliopiga simu za uongo katika Jeshi hilo mara kadhaa na kuomba huduma nyingine badala ya ajali ya moto hali iliyofanya Jeshi hilo kumkamata na kumhoji.
DUKA amesema yeye namba hiyo alipewa na mtu mwigine aliyedai kuwa mwenye namba hiyo huwa anatoa pesa za FREE MASON pia dawa za kienyeji kwa matatizo mbalimbali.

Hata hivyo DUKA alikiri kutenda kosa na kuomba msamaha kwa jeshi hilo ambapo aliachiwa huru na kisha kurejea kwao huku akijutia kosa  alilolifanya na kuahidi kutorudia tena

BONDIA WA KIMATAIFA FRANCIS MIYEYUSHO ASHAURIWA KUACHANA NA MAPAMBANO YA USWAHILINI KWANI YANASHUSHA HADHI YAKE!

Bondia Sadiki Momba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Miyeyusho wakati wa mpambano wao usiokuwa wa ubingwa uliofanyika siku ya jumapili katika ukumbi wa  Friends Coner  Manzese Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa pointi.
Bondia Sadiki Momba kushoto akioneshana umwamba wa kutupiana makonde na Fransic Miyeyusho wakati wa mpambano wao usiokuwa wa ubingwa uliofanyika siku ya jumapili katika ukumbi wa  Friends Coner  Manzese Dar es salaam Miyeyusho alishinda kwa pointi.
refarii Sako Mtlya akimnyoosha mkono juu bondia  Fransic Miyeyusho baada ya kumgalagaza Bondia Sadiki Momba wakati wa mpambano uliofanyika jana kwenye ukumbi wa Friend Conner Manzese.

SOMA KISA CHA MAMA ALIYEZITAFUNA NYETI ZA MWANAE KISHA KUZIMEZA!

  MKAZI wa Kijiji cha Mlongazila, wilayani Kisarawe, Pwani, Moshi Hamad anatuhumiwa kumng’ata mwanaye, Khadija Hamad (6) sehemu za siri kwa madai ya kujisaidia haja kubwa na ndogo hovyo.
  Wakizungumza kwa nyakati tofauti na Tanzania Daima juzi wilayani Kisarawe, wakazi hao walisema mama huyo amekuwa na tabia ya kumfungia ndani mtoto wake huyo na kumchapa kwa zaidi ya nusu saa, akitumia nyaya za simu na kumng’ata sehemu mbalimbali za mwili zikiwamo za siri na kumsababishia maumivu makali.
  Wakazi hao walisema waliamua kutoa taarifa kwenye dawati la haki za binadamu baada ya kuchoshwa na vitendo hivyo, na sasa wamelitaka Jeshi la Polisi kumkamata mama huyo na kumchukulia hatua.
  Stella Musa, alisema sehemu za siri za mtoto huyo zimeharibiwa kutokana na kung’atwa na meno, huku zikiwa na vidonda vinavyodaiwa vimetokana na kuchomwa na kitu chenye ncha kali. “Wazazi wa mtoto huyo ni wanangu, siku moja mama huyo alimuumiza mkono. Nilimchukua na kukaa naye nyumbani kwangu kwa mwezi mmoja nikimuhudumia kwa kumkanda kwa maji ya moto,” alisema Stella.
  Mwalimu wa Shule ya Msingi Mlongazila, Paulo Idana ambaye pia ni katibu wa dawati la kutetea haki za binadamu, alisema suala hilo limewafikia, hivyo wanachukua hatua za kisheria huku mtoto huyo amewekwa chini yao kwa matibabu zaidi.
  “Tulimfuata mama huyo Septemba 20 mwaka huu na tulifanya nae mahojiano mbele ya ofisa mtendaji wa kijiji na alikiri akisema alifanya hivyo kwa sababu ya hasira. Tunafanya utaratibu ili tumfikishe kwenye vyombo vya sheria,” alisema Idana.
  Akieleza mkasa huo, mtoto huyo alisema wakati mwingine mama yake alikuwa akimwita ili amfundishe kusoma na aliposhindwa aling’atwa mgongoni, mapajani na sehemu za siri huku akisema atamfanyia hivyo hadi ajue kusoma.
  Mama wa mtoto huyo, Moshi, alisema alikuwa akitoa adhabu kwa mwanaye huyo kutokana na kujisaidia haja ndogo na kubwa hovyo wakati akirudi shule.
  “Nafanya hivi kutokana na hasira siwezi nikamuona mtoto wangu anajisaidia haja kubwa na ndogo kwenye nguo nikamwacha tu, lazima nimwadhibu… jana alitapika kwenye sahani. Je, mtoto kama huyu nitamwacha?” alihoji Moshi. Mwenyekiti wa kitongoji hicho, Khadija Samizi alikiri kuwepo kwa tukio hilo.

NI KWELI NILIKAMATWA CHINA KWA SKENDO HII YA SASA, LAKINI NAMSHUKURU MUNGU NIMEYAMALIZA MWENYEWE WATANZANIA WA




                                      Rehema Fabian.

WAKATI msanii Agness Gerald ‘Masogange’ akisubiriwa kutua Dar baada kumaliza msala wake huko Afrika Kusini, skendo ya baadhi ya wasanii Bongo kuhusishwa na usafirishaji wa madawa ya kulevya ‘unga’, lingine limeibuka ambapo Video Queen Rehema Fabian amekiri kukamatwa nchini China kwa ishu hiyo.
Madawa ya kulevya.
Wiki mbili zilizopita kulizagaa habari kutoka kwa marafiki wa karibu wa Rehema ambao walidai kuwa mshiriki huyo wa Miss Kiswahili 2009 alikamatiwa huko Shaghai baada ya kukutwa na mwanaume aliyekuwa na unga.
Baadhi ya Watanzania waishio China walitofautiana ambapo wakati wengine wakidai kuwa alikamatwa na wapo waliosema kukamatwa kwake kulitokana na kupitiliza muda wa kuishi nchini humo tofauti na viza yake inavyoeleza.
Katika kipindi hicho chote, Ijumaa Wikienda limekuwa likimsaka ambapo wikiendi iliyopita lilifanikiwa kuchati naye ili kupata ukweli wa ‘niuz’ hizo.
Ijumaa Wikienda: Mambo vipi Rehema?

Rehema: Mambo poa tu. Nani mwenzangu?
Ijumaa Wikienda: Unachati na gazeti la Ijumaa Wikienda. Kuna taarifa zimezagaa Bongo kuwa umekamatwa na unga China. Hizi habari zina ukweli?
Rehema: Ni kweli nilikuwa mahabusu. Mateso ya huko wee acha tu. Nilipata kesi lakini si yangu ila namshukuru Mungu nimetoka salama.
Ijumaa Wikienda: Kesi inahusu nini na kama ilikuwa haikuhusu kwa nini ulikamatwa?
Rehema: Nilikamatwa na mtu (hakutaka kumtaja na ni nani kwake) alikuwa na unga, nimekaa mahabusu wiki mbili na siku mbili. Uzuri huyo mtu alikataa mbele ya polisi kuwa hanifahamu na sihusiki ndipo nikaachiwa.

WASIWASI WATANDA MSANII RAY KUSOMEWA ALALBADIR KUVIMBISHWA “BUSHA” KISA MKE WA MTU, ATAKIWA KUMUOMBA RADHI RAFIKI YAKE FRANK MTAO KUHUSU MKEWE, CHUCHU HANS APIGWA TARAKA!

 Frank Mtao ambae amedaiwa kumpa taraka mkewe Chuchu Hans kisa  rafiki yake Ray
 Msanii Ray akiwa kwenye majukumu ya kuigiza
  Chuhu Hans





 Moja ya Layout ya gazeti pendwa liliripoti habari ya fumanizi la Ray na Chuchu Hans.

 Chuchu Hans akiwa na mtoto wake


Na Mwandishi Wetu
Ni kipindi kirefu sasa kumekuwa na madai ya kashfa ya msanii Vicent Kigosi “Ray “ kudaiwa kuwa na mahusiano ya kimapenzi  na mke wa mtu ambae pia ni msanii wa bongo muvi Chuchu Hans huku vyombo mbalimbali vya habari hasa magazeti pendwa yakiripoti kwa kina tukio hilo.
Habari za ziada zilizonaswa na Xdeejayz toka kwa mtu wa karibu na familia ya Frank Mtao zilisema kuwa taarifa za Ray kutembea na Chuchu Hans zinaukweli kubwa sana kwani hata tukio la hivi karibuni la Ray kufumaniwa na akiwa na Chuchu Hans wanazichukulia kama ni za ukweli kwani Johari ambae ndiye mchumba harisi wa Ray aliwahi kukutana na mmoja wa wanafamilia wa Frank Mtao na kuwaeleza kila kitu.
Hata hivyo  Ray  inadaiwa amesababisha ndoa ya Frank Mtao kuvunjika kwani hivi karibuni Frank Mtao ambae anaishi nchini Austaralia baada ya tukio la kufumaniwa mkewe na Johari akiwa na Ray nyumbani kwa Chuchu mtangazaji huyo amemtwanga taraka Chuchu Hansa ambae sasa hivi maisha yanamwendea kombo baada ya kushindwa kulipia pango ya nyumba maeneo ya Msasani na kuhamia Mwananyamala kwa Mama Zacharia uswahili.
Aidha  katika hali isiyokuwa ya kawaida Ray anadaiwa amekuwa akimng’ong’a Frank Mtao kwa kujifanya kuwa ni rafiki yake wa karibu  na mara nyingi amekuwa akimpigia simu Frank Mtao na kumuweka roud speak wakati akiwa na Chuchu Hans.
Chanzo hicho kiliendelea kueleza “ Kwa kweli inasikitisha kuna siku Ray alikuwa na Chuchu Hans alimpigia simu Frank Mtao na kuanza kutaniana nae na baadae alimuuliza kama huko hana demu  na Frank alimjibu kuwa anae wa kuzugia na Ray alihitaji Frank amtumie picha yake na Frank alifanya hivyo na picha hiyo aliiona Chuchu Hans na baadae palizuka mtiti mzito” Alisema dada huyo ambae alisema yeye ni binamu wa familia ya Frank.
Aidha watu mbalimbali wameonesha wasiwasi wao kuwa huenda Frank Mtao akalipa vibaya kwa kumsomea alalbadir msanii Ray na kama kweli tuhuma anazotuhumiwa zitakuwa za kweli msanii huyo atakuwa amejipatia matatizo makubwa kutokana na dua hiyo jinsi inavyofanya kazi kama tukio lina ukweli na huenda akashushwa “busha” na baadae atalazimika kutembea na mkwangwaju.

MSICHANA MREMBO KULIKO WANAWAKE WOTE DUNIANI ACHUKUA TAJI LA UREMBO WA DUNIA, JARIBIO LA WAISLAM WENYE ITIKADI KALI WASHINDWA KUVURUGA ONESHO!


Mrembo wa Duinia 2013, Megan Young wa Philippines baada ya kutwaa taji hilo.
Mrembo wa Duinia 2013, Megan Young  (katikati) wa Philippines akiwa na mshindi wa pili Marine Lorphelin (kushoto) wa Ufaransa, na mshindi wa tatu Carranzar Naa Okailey Shooter (kulia) kutoka Ghana.
Warembo mbalimbali walioshiriki shindano hilo.

MREMBO wa Philippines alivishwa taji la binti mzuri zaidi duniani mwaka huu (2013) jana huko mjini Bali, Indonesia, ambapo kulikuwa na wasiwasi kwamba Waislam wenye msimamo mkali walikuwa wamedhamiria kulivuruga tukio hilo.
Mlimbwende huyo, Megan Young, mwenye umri wa miaka 23, aliyezaliwa Marekani, ambaye anachukua mafunzo ya upigaji wa filamu, alipokea taji la mashindano hayo kutoka kwa mshindi wa mwaka jana, Wenxia Yu wa China, na akaahidi kuwa “mlimbwende bora zaidi duniani ambaye hajawahi kutokea".
Maelfu ya Waislam wa chama cha Islam Defenders Front waliingia mitaani tangu mwezi uliopita wakipinga kufanyika kwa mashindano hayo nchini Indonesia, nchi ambayo ina Waislam wengi zaidi duniani, wakiyaita mashindano hayo kuwa ni “maonyesho ya ngono”.
Upinzani huo uliwalazimisha waandaji kulihamisha tukio hilo kutoka Jakarta kwenda Nusa Dua, kusini mwa Bali.
Katika kulifahamu hilo mapema, balozi za Marekani, Uingereza na Australia zilitoa vibali vya kwenda kwenye shindano hilo kwa kuwaonya wenye kusafiri kwamba tukio hilo la mashindano ya urembo lilikuwa limepangwa kuvurugwa. Hata hivyo, polisi wa Indonesia walisema hapakuwepo na vurugu zozote siku ya Jumamosi.
Marine Lorphelin, mwenye umri wa miaka 20 kutoka Ufaransa, alishika nafasi ya pili na Carranzar Naa Okailey Shooter (23) kutoka Ghana alikuwa wa tatu.

MH.MBOWE APATA PIGO KUBWA DADAAKE ALIYEHAMIA CCM TOKA CHADEMA AFARIKI GHAFRA NJIANI!

 
DADA wa Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe, amefariki papo hapo baada ya gari alilokuwa akiendesha kupasuka tairi ya mbele na kuingia chini ya daraja baada ya kupinduka na kusababisha watu wawili kufa na wengine watatu kujeruhiwa vibaya.

Dada huyo, Grace Aikaeli Mbowe,  anayesadikiwa kuwa na umri kati ya miaka 47 hadi 50, alikuwa akiendesha gari yenye namba T 277 CAJ aina ya Toyota Cresta akiwa na mumewe  aliyefahamika kwa jina la Ibrahim Lukindo (52), wakitokea Jijini Tanga, walipata ajali hiyo eneo la Kabuku wilayani Handeni.


Kamanda wa polisi mkoani Tanga (ACP) Costatine Massawe alisema kupitia Ofisa wake wa upelelezi mkoani Tanga, Bw Aziz Kimata, kwamba ajali hiyo ilitokea majira ya saa 1:30 asubuhi jana  katika eneo hilo baada ya gari hilo kupasuka tairi ya mbele kulia na kisha kuingia chini ya daraja lililokuwepo eneo hilo.

"Ni kweli kuna ajali ilitokea eneo la Kabuku gari aina ya Cresta lililokuwa likiendeshwa na ndugu inavyosemekana wa Bw Freeman Mbowe, limepata ajali baada ya kupasuka tairi la mbele na kuacha barabara na kuingia chini ya daraja .


"Dereva anayeitwa Grace Aikael Mbowe na mtu anayesemekana ni mumewe anayeitwa Ibrahim Lukindo, wamefariki na watu watatu waliowachukua wamejeruhiwa," alisema RCO Kimata.

Aliwataja waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na Bw Ridhiwani Bakari (29) aliyekuwa na mkewe Zeddy Nzuke (29) raia wa Kenya aliyekuwa na mtoto wake mwenye umri wa miaka miwili na miezi minne aliyefahamika kwa jina la Mariam Ridhiwan ambao kwa sasa wamelazwa katika hospitali ya Magunga wilayani Korogwe.

 
RCO Kimata aliyezungumza kwa niaba ya kamanda huyo wa polisi alisema chanzo cha ajali hiyo inasemekana kimetokana na kupasuka kwa mpira huo na mwendo kasi wa kawaida na kwamba majeruhi na maiti zimehifadhiwa kwenye hospitali hiyo.
 
Mwandishi wa habari hizi, aliyefika kwenye hospitali hiyo na kuzungumza na Ridhiwani pamja na mkewe ambaye amelazwa wodi namba mbili ya wanawake katika hospitali hiyo, alisema kwamba ndoto zake za kufanya kazi Dar es salaam zimezimika ghafla kutokana na kwamba alikuwa aende kupamba kazi ya uofisa ugavi katika taasisi moja ya fedha ya marehemu Mbowe Jijini Dar es salaam.
 
"Nilikuwa naenda kupewa kazi na mama Mbowe katika Institution yake ya Micro-Financial Jijini Dar es salaam, mimi ni procurement (Mgavi-manunuzi) na ni Mkenya kwetu ni Eastern Province Kang'undo na nimeolewa na bwana Mtizedi...Lakini sasa ndoto zangu za kufanya kazi Dar es salaam zimezimika ghafla," alisema Zeddy akiwa kitandani amelala na mwanwe ambaye alikuwa haongei tangu amefika katika hospitalini hapo.
 
Mumewe na mwanamke huyo akizungumzia ajali hiyo alisema kuwa hakuwa akijua kwani alikuwa amelala dakika tatu kabla ya kutokea ajali hiyo ambapo alishtukia yeye, mkewe na mwanawe wametupwa chini kwenye majani wakiwa hawajijui na walikimbizwa katika hospitali hiyo ya Korogwe
 
Ridhin ambaye ni mkazi wa Nguvumali Jijini Tanga, alisema safari yao hiyo ilikuwa ifanyike Jumamosi mchana lakini kutokana na na kuchelewa kwa wenyeji wao hao, waliondoka Tanga kwenye hoteli ya Doliphin walikolala majira ya saa 11:00 alifajiri kwa ajili ya kwenda Jijini Dar es salaam.
 
Muuguzi wa zamu wa hospitali hiyo Bi Nayela Missingo alikiri kuwapokea wagonjwa hao ambapo alisema wanafanya jitihada za kuwahamishia katika hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es salaam mtoto Mariam ambaye amepata majeraha katika kichwa chake na kwamba tangu afikishe hospilaini hapo hakuwa katika hali nzuri, haongei walakunyonya.


 
  Bi Zeddy Nzuke  na mtoto wake wakiwa wamelazwa katika hospitali ya Magunga wilayani Korogwe baada ya kupata majeraha katika ajali hiyo

WANANCHI WAMPONGEZA MKUU WA WILAYA ALIYEWAPIGIA MAGOTI WANANCHI WAKE KUONESHA UNYENYEKEVU, VIONGOZI WENGINE WATAKIWA KUIGA TABIA HIYO!

 
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi8dysIPBzfJjyDfTAIhGw0Jwu8x41xUZNhGMHrEEq7YVCF3ESNZZOj0ZvJPtCE5jxXSktDofI_V0-y9tZ-K8VYaGGcqhx2716Dcfoxj_ieyQhR1R7SojrG2Z3VN2hHEmKreTUtmRF5fklA/s1600/dc.jpg
Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, mkoani Manyara, Anatory Choya akiwa amewapigia wananchi magoti kwa maana ya kuonyesha unyenyekevu
Mbulu. Mkuu wa Wilaya ya Mbulu, mkoani Manyara, Anatory Choya, amesema kuwa aliwapigia magoti wananchi wa Kijiji cha Hydom, ili kuonyesha unyenyekevu kwa wananchi hao aliodai walionekana kujazwa maneno ya uchochezi na wanasiasa ili wavuruge amani .

Alisema kutokana fujo zilizofanywa na baadhi ya wananchi hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika majuzi, kwa nafasi yake angeweza kuagiza hata Jeshi la Polisi kuwadhibiti watu, lakini misingi ya dini yake haimruhusu kumdhuru mtu zaidi ya kumwonyesha unyenyekevu.
 
 

Alisema hali hiyo ndiyo iliyomfanya kuamua kupiga magoti na kumshtakia Mungu.

“Mimi ni mkristo, unyenyekevu ndiyo nguzo pekee ya kuonyesha upendo na kudumisha amani. Ningeweza kuagiza polisi wawadhibiti, lakini sioni sababu kwa kuwa hiyo siyo misingi ya utawala. Ndiyo maana nikaona bora nitumie njia nyingine ya kumshirikisha Mungu mbele yao,”alisema Choya na kuongeza:

“Wanasiasa wamekuwa wakipandikiza chuki kwa wananchi kwa makusudi kwa lengo la kuvuruga amani lakini kwa kumweka Mungu mbele nina imani tutafanikiwa ili siku moja tusije tukaingia kwenye mkumbo wa Syria na Misri”

Choya alitoa kauli hiyo jana alipokuwa akizungumza na Mwananchi Jumapili, siku chache baada ya kitendo chake cha kupiga magoti mbeye ya wananchi kwenye mkutano wake wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Haydom.

Mkuu huyo wa wilaya alidaiwa pia kuwalaani baadhi ya wakazi wa Kijiji cha Haydom kwa kile kinachodaiwa kuwa ni kumdharau na kutofuata maagizo yake, wakati yeye amewasaidia katika kutatua migogoro mbalimbali waliyokuwa nayo.

Tukio hilo la kusikitisha lilijitokeza baada ya wananchi wa kijiji hicho kupinga agizo la Choya, lililowataka kufanya uchaguzi wa kaimu mwenyekiti wa kijiji hicho, kabla ya kufanya uchaguzi mdogo, ambapo walipinga kwa kudai kuwa hakuna sheria hiyo.

Mmoja wa wananchi hao alilumbana na mkuu huyo wa wilaya mbapo Choya alijibu; “Nami nitarudi kwetu." Naye Tikin akasema tena: “Unasema utarudi kwenu Biharamulo wakati hawakutaki kwani ulifukuzwa ubunge?”
Maneno hayo yalionyesha kumkwaza Choya ambapo alipiga magoti huku machozi yakimlenga na kumwomba Mungu afanye jambo kwa watu wa Haydom kwani wanamdharau kabla ya kujitokeza wazee watatu wa Haydom na kumwomba msamaha mkuu huyo wa wilaya

Sunday, September 29, 2013

MAJAMBAZI WAFANYA UMAFIA BENKI DAR, WAPORA ZAIDI YA TSH 150, WALIINGIA WAKIWA NA SARE ZA POLISI KUWAZUGA WAFANYAKAZI!




Majambazi saba akiwemo mmoja ambaye amevalia sare za polisi wameiteka benki ya I&M  jijini Dar es Salaam na kuchukuwa fedha zinazohisiwa  kuwa  ni zaidi ya shilingi milioni 150 na kutokemea kusikojulikana.
Tukio hilo limetokea katika benki hiyo iliyoopo katika makutano ya mtaa wa Indira Gandi na Mosque ambapo baadhi ya mashuhuda wameelezea tukio hilo lilivyokuwa.
 
Akizungumza katika eneo la tukio kamanda wa polisi mkoa wa Ilala kamanda Marieta Minagi amesema bado wanaendelea kufanya uchunguzi wa tukio lenyewe ingawa  mpaka sasa ni kama milioni zaidi  150 zinahisiwa kuibiwa.
 
Naye mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Said Meki Sadiki akiwa katika eneo hilo amesema  matukio ya Kuiba fedha katika benki yanazidi kushamiri na hivyo kuna haja ya taasisi husika kujipanga  upya.
  Hata hivyo ITV ilishuhudia baadhi ya wafanyakazi wa benki hiyo wakipandishwa katika gari la polisi lenye namba za usajili  T220 AMV na kuondoka  nao kwa ajili ya mahojiano  zaidi

JAMANI WAUME WA WATU NI SUMU ACHANENI NAO KABISA, ONENI DADA HUYU ALIVYOPIGWA NYEMBE KWENYE SHAVU BAADA YA KUFUMANIWA NA MUME WA SHOSTI WAKE!



Hawa  ni  mabinti  wawili  ambao  walikuwa  ni  marafiki wa  damu.Urafiki wao uliingia  dosari  baada  ya  mabinti  hao  kusalitiana  na  kuchukuliana  wapenzi....

Anayevuja  damu  usoni ni  binti  ambaye  amechanwa   nyembe  na Magreth  ( rafiki yake ) akimtuhumu  kutembea  na  mpenzi wake.


MAJAMBAZI WALIOMVAMIA FEZA KESSY KUMBE WALITUMWA NA MAADAU WAKE KUMFANYIA KITU MBAYA!




  Siku ya jana mitandao kadhaa ya kijamii ilitaarifa habari ya kusikitisha ya aliyekuwa mshiriki wa Big Brother da Chase Feza Kessy baada ya kuvuamiwa na majambazi wenye silaha nzito, hivyo wasomeji wengi walielezea tukio hilo huenda ni la utengeneza na wabaya wake waliokuwa na nia ya kummalizi.
Feza Kessy  alipatwa na matatizo ya kuvamiwa na majambazi wenye silaha siku mbili zilizopita. Feza Kessy amesema kwamba tangu avamiwe na majambazi hao hajisikii kuwa na amani kabisa. Feza Kessy anaendelea kuwashangaa hao majambazi kwamba silaha walizobeba zilikuwa za nini?, au walidhani kwamba anapesa wakati hakushinda Big brother na alikuwa hana kazi kwa muda miezi mitatu iliyopita. Pole sana Feza Kessy na hizi ni tweet zake akielezea tukio hilo

MASKANI SERIKALI YAYAFUNGIA MAGAZETI YA MWANANCHI NA MTANZANIA KUTOCHAPISHA HABARI ZAKE TENA!


Serikali imeyafungia kutochapishwa Magazeti ya MWANANCHI na MTANZANIA kuanzia 27 Septemba, 2013 kutokana na mwenendo wa magazeti hayo kuandika habari na makala za uchochezi na uhasama kwa nia ya kusababisha wananchi wakose imani kwa vyombo vya dola hivyo kuhatarisha amani na mshikamano uliopo nchini.
Gazeti la MWANANCHI limefungiwa kutochapishwa kwa siku kumi na nne(14) kuanzia 27 Septemba,2013. Adhabu hii imetangazwa kwa Tangazo la Serikali (Government Notice ) Namba 333 la tarehe 27 septemba,2013.
Gazeti la MWANANCHI limepewa adhabu hiyo kutokana na hivi karibuni kuchapisha habari zenye mwelekeo wa uchochezi na uvunjifu wa amani, mfano tarehe 17 Julai, 2013 katika toleo Namba 4774 ilichapisha habari isemayo “MISHAHARA MIPYA SERIKALINI 2013” kwa kuchapisha waraka uliozuiliwa kwa matumizi ya vyombo vya habari waraka huo ulikuwa wa Siri haukupaswa kuchapishwa Magazetini. Aidha, katika toleo la Jumamosi, tarehe 17 Agosti,2013 lilichapisha habari yenye kichwa kisemacho “WAISLAM WASALI CHINI YA ULINZI MKALI” habari hiyo ilikolezwa na picha ya Mbwa mkali mwenye hasira. Habari na picha hiyo ilitoa tafsiri ya kuwa Jeshi la Polisi lilipeleka Mbwa katika maeneo ya ibada ya waumini wa dini ya kiislam. Jambo ambalo halikuwa la ukweli. Jeshi la Polisi katika doria siku hiyo halikupeleka mbwa katika maeneo ya Misikiti.
Serikali na jeshi la Polisi linaheshimu na kuzingatia maadili ya dini ya Kiislamu na kwa hiyo Jeshi lake hakiwezi kupitisaha au kuingiza Mbwa katika maeneo ya ibada. Hivyo basi, kwa gazeti hili kuchapisha habari iliyokolezwa na picha ya mbwa ni uchochezi wa kulichonganisha Jeshi la Polisi na waumini wa dini ya kiislam mbwa ni najisi hapaswi kuingia katika maeneo ya ibada.
Gazeti la MTANZANIA limefungiwa kutochapishwa kwa siku tisini(90) kuanzia tarehe 27 Septemba,2013 kwa kuchapisha habari zenye uchochezi. Gazeti hili limeonywa mara nyingi lirekebishe mtindo wake wa uandishi wa kichochezi na lizingatie maadili na Sheria na Kanuni za fani ya Habari.
Pamoja na kuonywa gazeti hili halikuonyesha kuzingatia maelekezo ya Msajili wa Magazeti, mfano; Katika toleo na 7262 la 20 Machi, 2013 liliandika habari yenye kichwa kisemacho “URAIS WA DAMU”, tarehe 12 Juni, 2013, toleo Namba 7344 lilichapisha makala isemayo “MAPINDUZI HAYAEPUKIKI”. Aidha, siku ya Jumatano,tarehe 18 Septemba,2013 katika toleo Namba 73414 ukurasa wa mbele lilichapisha Kichwa cha habari kisemacho “SERIKALI YANUKA DAMU” taarifa hiyo ilikolezwa na picha zilizo unganishwa kwa ustadi mkubwa kwa kutumia kompyuta kutapakaza rangi nyekundu mithili ya damu nyingi kumwagika. Katika habari hiyo gazeti hilo limedai bila uthibitisho kuwa Jeshi la Polisi linahusika na wahanga walioumizwa na watu wasiojulikana kwa kumwagiwa tindikali na waliyovamiwa na kujeruhiwa vibaya.
Vile vile gazeti hilo limeishutumu serikali kuwa goigoi katika kushughulikia matukio yenye sura ya kigaidi. Kwa ujumla wake habari hiyo ni ya kichochezi ina lengo la kuwafanya wananchi wavichukie vyombo vya ulinzi na usalama wavione kuwa haviwasaidii.
Kutokana na makosa yalitajwa hapo juu serikali imelifungia gazeti la Mtanzania kutochapishwa kwa muda wa siku tisini (90) kwa Tangazo la Serikali Namba 332 (Government Notice No.332) la tarehe 27 Septemba, 2013,. Serikali inawataka wamiliki, wahariri na wanahabari kwa ujumla kuwa makini, kuzingatia weledi,miiko na madili yataaluma uandishi wa habari.
Serikali inawataka wamiliki na hasa wahariri kuhakisha kuwa habari wanazoziandika na vipindi wanavyoviandaa vinazingatia taaluma, kuweka mbele maslahi ya taifa letu kwa kuwa na uzalendo wa hali ya juu. Serikali inavionya vyombo vya habari vinavyoutumia uhuru wa habari bila wajibu kuwa haitasita kuvichukulia hatua kali ikiwemo ya kuvifungia. Serikali haitakubali kuona vyombo vya habari kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani nchini.
Imetolewa na;
MKURUGENZI IDARA YA HABARI WIZARA YA HABARI, VIJANA, UTAMADUNI NA MICHEZO 28 SEPTEMBA, 2013

Friday, September 27, 2013

RAY C AHAIDI KUMPA URODA WA BURE KWA MTOTO WA WAZIRI AMBAE ALISAIDIA KUOKOA WATU WENGI WAKATI WA MASHAMBULIZI YA KIGAIDI WESTGATE KENYA, HUENDA AKAENDA KWA AJIRI YA KUTIMIZA AZMA YAKE HIYO!





Abdul Haji ni miongoni mwa mashujaa ambao hawatasahaulika nchini Kenya kutokana na kuamua kuhatarisha maisha yao ili kuokoa watu waliokuwa wamekwama ndani ya jengo la Westagate baada ya kushambuliwa na Al-Shabaab Jumamosi iliyopita.
Tangu asimulie namna alivyopambana na magaidi hao, Haji ametokea kuwa kipenzi cha watu wengi hasa wasichana na mmoja wa watu aliowagusa ni Rehema Chalamila ambaye amesema anatamani mwanaume mjasiri kama yeye ambaye watazaa naye watoto.
“In love with ths Soldier!i want a soldier like him to marry me,” ameandika Ray C kwenye picha ya gazeti aliyoipost kwenye Instagram ikimuonesha Abdul Haji.
“I love You Abdul Haji,You are my Heroooooooo,” aliandika Ray C kwenye picha nyingine.
Kwenye picha nyingine Ray C aliongeza, “My soldier,My Prince,My Love….Love You Abdul Haji.”
Kijana huyo ni mtoto wa waziri wa zamani wa ulinzi nchini Kenya ambaye alienda kwenye mall hiyo baada ya kupata ujumbe kutoka kwa rafiki yake kuwa kaka yake alikuwa ndani ya Westgate wakati watu hao wenye silaha walipovamia.
Akiongea na NTV, Haji ambaye sio mwanajeshi, alisema alifundishwa kutumia bunduki na baba yake ili kulinda mifugo yao isiibiwe na wezi.
Ujuzi huo ulimsaidia Jumamosi hiyo kuwasaidia wafanyakazi wa Red Cross wafanye kazi yao kwa usalama kwa saa tatu na kusaidia kuokolewa kwa watu wafikao 1,000 nje ya mall hiyo

POLISI WALIYEMPIGA SHOGA NA KUMDHALILISHA WAZUSHA BALAA, MASHOGA WAANDA MAANDAMAMO MAKUBWA WAKIWEMO TANZANI!


Na Xdeejayz kwa msaada wa mtandao.
Shoga  moja  nchini  Nigeria  limejikuta  likiangukia  mikononi  mwa  polisi  wa  nchini  hiyo  baada  ya  kujifanya  ni  DEMU...
Shoga  hilo  lilikuwa  na  mazoea  ya  kuvaa  nguo  za  kike  na  urembo  mwingine  wa  kike  ikiwa  ni  pamoja  na  keseti  nywele  zake  ili  kuwarubini  wanaume....
Kwa  kifupi  ni  kwamba, ukiliona  ni lazima  ULIMEZEE  MATE...Likivaa  nguo  za  kike,...linapendeza  kuliko  hata  wanawake...
Nyuma  limefungasha  kiaina  ( choo kipo )  na  kifuani  huweka  matiti ya  bandia...Ukilitongoza  ujue  utapewa KABANG ( kiboga )  , maana  ni  dume  hilo.
Wanaume  ambao  si  wadau  wa  KABANG, waliamua  kulilipoti  polisi  ambapo  lilikamatwa ...
Mateso  aliyopewa  huyu  shoga, nadhani  hatakaa  ayasahau  maishani  mwake..
Hata hivyo tukio limeonekana kuwa kera mashoga wote duniani wakiwemo wa hapa nchini Tanzania hivyo wametishia kufanya maandamano makubwa.
Kwa mujibu wa mtandao mmoja nchini humo. 

FILAMU YA UFUSKA YA MSANII MANAIKI SANGA YAVUNJA REKODI SASA YAFIKIA ODA KOPI ELFU 38 NCHI NZIM, KAMPUNI YA USAMBAZAJI YA STEPS YAVUJISHA SIRI NZITO!!

Na Mwandishi Wetu.
Katika hali ya kushtua kuna taarifa kuwa filamu ya msanii kina kwa ufuska kwenye kiwanda cha bongo movie Manaiki Sanga "The Don" ameweka rekodi mpya nchini kufuatia filamu yake kufikisha kopi nyingi ambazo huenda kiasi hicho hakijawahi kufikiwa na msanii yeyote.

Habari za uhakika toka kwa mtu wa karibu na kampuni ya Steps ambae aligoma kutaja jina lake kwa madi kuwa yeye si msemaji wa kampuni hiyo alisema " Kwa kweli hii ni kali unajua hadi sasa hapa ofisini tunapokea maelfu ya filamu wakihitaji kupata nakala ya filamu ya msanii huyo" Alisema kijana huyo wa kihindi

Aidha kijana huyo aliongeza kusema kuwa kitu kikubwa kinachofanya watu kuisubiri kwa hamu filamu ni kutaka kuona msanii huyo aliyejizolea umaarufu nchini na dunia nzima kutokana na picha za utupu za mabint zaidi ya 400 ambao baadae hao mabint  wote kuwafanyisha filamu hiyo inayoitwa Ngema huku pia mastaa mbalimbali wakishirikishwa.
Kijana huyo alimaliza kusema kampuni ya Steps imeichukua filamu hiyo na tayari wako kwenye makubaliano ya mwisho na Manaiki na huenda ikapewa nafasi ya kuachiwa haraka mtaani kutokana na wananchi wengi nchini Tanzania na Kenya, Kongo na Uganda kutaka filamu hiyo kuwafikia ili kuona nini kilichopo ndani yake.