TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Thursday, June 9, 2016

MGANGA WA MASTAA AITWA NCHINI MAREKANI, WAZUNGU WAPAGAWA NA DAWA ZA MITI SHAMBA ANAZOWAPATIA WA2. WASEMA TANZANIA YATAKIWA KUJIVUNIA KIPAWA ALICHOKUWA NACHO..!

 Dokta Kamdege maarufu kama Mganga wa mastaa akiwa kwenye ufisi yake Mkoani Tabora Wilaya ya Sikonge kijiji cha Lukanga
  Dokta Kamdege maarufu kama Mganga wa mastaa akiwa kwenye ufisi yake Mkoani Tabora Wilaya ya Sikonge kijiji cha Lukanga
 Dokta Kamdege maarufu kama Mganga wa mastaa akiwa kwenye ufisi yake Mkoani Tabora Wilaya ya Sikonge kijiji cha Lukanga. huku kwa juu kukionekana kama antena ambazo maalum kwa kunasa watu wenye hila mbaya.
 
Na Shabani Fugusa- Tabora
Mtaalamu wa miti shamba Tanzania anaetambuliwa na chama cha waganga wa tiba za asili Tanzania na mwenye leseni Dokta Kamdege hivi karibuni ataondoka nchini kuelekea nchini Marekani kwa ajiri ya kwasaidia watu wa huko kwenye maradhi mbalimbali yanayowasumbua.
Akiongea na maskanibongotz toka Tabora mganga huyo alisema kuwa baada ya kufanikiwa kuwaagua wazungu wengi kwa dawa zake za miti shamba hatimae amepewa mwariko wa kwenda nchini huko.
Aidha Dokta Kamdege ambae pia amekuwa akitumiwa sana na baadhi ya viongozi wa vyama na mastaa wa bongo movie kuweka sawa mambo yao kwa kutumia miti shamba tu hivi karibuni alitingisha jiji la Bunjumbura kwa kuwasaidia wagongwa walishindikana.
Dokta Kamdege amekuwa akitumia miti shamba kuwasaidia watu walikwishafanyiwa mambo ya kichawi katika maisha yao na kukosa mafanikio, kupandishwa vyeo, kujikinga na wachawi, kung'arisha biashara na kuwa na nyota ya ajabu kwenye mambo yote unayoyafanya katika maisha yako kiasi cha kuwashangaza watu wanaokuzunguka.
Aidha Dokta Kamdege amefanikiwa kuwasaidia hata waliokuwa hawapati watoto au kupata wachumba, kukosa mafanikio licha ya kufanya kazi sana lakini kipato hakionekani, hali hiyo imepelekea Mkoa wa Tabora kuwa na ongezeko la watu wanaofika kwake kupata tiba hizo na kusafishwa kupitia miti shamba tu na sio uchawi kama wanavyofanya waganga wa mjini.
Kamdege alisema kama yupo anaehitaji msaada kwenye mtatizo aliyoyaanisha hapo juu basi apige simu hizi 0763-146231, 0788-844490 na ataongea na yeye moja kwa moja na sio lazima usafiri kumfuta Tabora hapana huko huko aliko atakusaidia...!

Wednesday, June 8, 2016

RC PAUL MAKONDA KIBOKO, APEWA SHAVU JINGINE LA MAANA, WAZEE NA VIONGOZI WA DINI MKOA WA DAR WATOA KAURI NZITO.



 BAADHI YA WANANCHI WALIPOTEZA NDUGU ZAO WAKIWA NA MABANGO YA KUMPONGEZA RC MAKONDA KWA JUHUDI ZAKE ZA KULETA AMANI ENEO HILO.
 RC MAKONDA AKIWA AMEZUNGUKWA NA MABANGO KIPINDI AKIWA MKUU WA WILAYA YA KINONDONI MWAKA JANA.
RC MAKONDA AKIWA MTAA WA NYAKASANGWE KWENYE MOJA YA MIKUTANO YAKE KWENYE UTATUZI WA MGOGORO WA ARDH KATI YA WANANCHI NA MAFISADI WA ARDHI.


 JOYCE ASENGA MWANAHARAKATI ASIYEKUWA NA CHAMA AMEMPONGEZA RC MAKONDA KWA UTENDAJI WAKE KAZI HASA KWENYE UTETEZI WA WATU WANYONGE AMBAO WALIKUWA WAMEKOSA MATUMAINI NA SERIKALI YAO.

Na Livingstone Mkoi
 Nyota ya mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda imeendelea kung'ara baada ya wakazi wa kata ya Wazo mtaa wa Nyakasangwe na Nyakalekwa kuiomba Manispaa ya Kinondoni kuruhusu mitaa hiyo kuitwa jina la Makonda kutokana na kazi kubwa aliyoifanya wakati akiwa mkuu wa Wilaya hiyo.

 Wakiongea na Maskanibongotz/ Sadicktv wakazi wa maeneo hayo kwa nyakati tofauti walisema ‘Mheshimiwa Makonda amefanya jambo kubwa sana  kurejesha amani  iliyokuwa imepotea hadi kusababisha maafa kwenye mgogoro wa ardhi katika eneo letu’ , eneo hilo awali lilikuwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe kwa kutumia siraha za jadi kama mishale, mapanga na visu baina ya watu wanaosadikika kumiliki maeneo makubwa na wakazi ambao wamekuwa wakiishi hapo kwa muda mrefu,kitu ambacho kilipelekea hata jeshi la Polisi kushindwa kuthibiti kwa wakati.

Baada  ya kuteuliwa Ukuu wa Wilaya ya Kinondoni, Paul Makonda  ziara yake ya kwanza ilikuwa eneo hilo ambapo siku ya kwanza alifika katika eneo hilo na gari zisizopungua saba za Polisi na kufanya mkutano ambapo aliwaaahidi wakazi hao kuwa atapigana kufa na kupona kuhakikisha wakazi hao wanapata haki yao ya kupata ardhi lakini na kurejesha amani iliyokuwa imepotea.

 Makonda alianza kuunda kamati iliyoshirikisha sehemu tatu, moja ilikuwa ni ya watu wanaojifanya wenye mashamba, mbili ya wakazi wa eneo hilo na tatu iliyokuwa chini yake na baadaye alikaa chini kukubariana wafanye uhakiki kwanza wa maeneo hayo ili kubaini ni kweli watu hao wenye mashamba wanachokisema kuhusu ukubwa wa maeneo yao ni sahihi.

Zoezi la kuhakiki lilianza mwaka jana lakini ikabainika madudu makubwa kwani watu wanaosema hayo ni mashamba yao walionekana kufanya udanganyifu wa hali ya juu kwa kile kilichoonekana kwamba wamejiongezea maeneo kinyemela tofauti na vile ambavyo inaonyesha katika michoro, hivyo kupelekea kazi sasa kuwa rahisi kugawa haki kwa wakazi wa eneo hilo.

 Hata hivyo  zoezi hilo kwa sasa limesimama tangu Makonda apande cheo huku wananchi wote wa eneo hilo masikio yao, macho yao na akili  zao zipo kwa Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ndiye wanayemtegemea kutatua tatizo hilo, huku wakiamini ya kwamba hatua kali zitachukuliwa dhidi ya watu hao wenye mashamba kwa mambo matatu, la kwanza walisababisha mauji ya watu saba wakati wa mapambano kipindi walichokuja kuvunja eneo hilo, na suala jingine ni nani aliyewapa mamlaka ya kuwavunjia watu nyumba zao pamoja na kuharibu mali zao zenye thamani ya mabilioni ya pesa na la mwisho uongo wa kumdanganya Makonda na vyombo vya sheria.
Kwa sasa hali ni shwali katika eneo hilo, kinachosubiriwa ni hatua zichukuliwe dhidi ya waharibifu, lakini amani ambayo wanaipata Wananchi wa eneo imewafanya watoe ya moyoni kwamba pasipo Paul Makonda hawajui mpaka leo wangekuwa katika hali gani ‘Tulijiona si Watanzania tena, Makonda ametufanya tufurahie amani ya nchi yetu, kwa sasa tunaishi kwa amani sana, tunaomba Serikali itusikie, hatuna cha kumpa Makonda, lakini ni heshima kwetu kuona eneo hili linapewa jina lake, hii itatosha kuwaambia watu wote na vizazi vijavyo kazi nzuri aliyotufanyia Kijana huyu’, walisema Wazee wa eneo hilo.

Katika hatua nyingine Viongozi wa Dini wa eneo hilo, wamesema ya kwamba kuna wakaTI Mungu anawatumia watu wake kuokoa, kwa nyakati tofauti Viongozi hao wamesema unaposoma maisha waliyoishi mitume na manabii, utapata kuona jinsi ambavyo walitumwa na kupambana pale inapotokea kwamba eneo fulani linakosa amani, eneo hili awali Mkuu wa Mkoa aliyepita Mecky Sadick alikuja lakini hakuweza kumaliza tatizo, tumeona alichofanya Paul Makonda, tunasema huyu alitumwa kuhakikisha anarejesha amani ya Nyakasangwe na Nyakalekwa, tunamuombea kwa Mungu na hakika anastahili heshima hii ambayo wakazi wa eneo hili wameamua kumpa.
Source Maskanibongotz

Sunday, June 5, 2016

MIUJIZA YA MCHUNGAJI MZOLA YAWASHANGAZA MADAKTARI BINGWA, WENYE UKIMWI, UKICHAA WAPOKEA UPONYAJI WA PAPO HAPO, WAGUMBA NAO WAPATA WATOTO, WATU WAZIDI KUMIMINIKA HATA NAFASI ZA KUKAA HAKUNA...!

 Mchungaji Mzola wa Kanisa la Hosana Msigani maarufu kwa jina la  NGOMA YA YESU MSIGANI lililopo Wazo Jijini Dar
 Mmoja wa wagonjwa ambae ameacha kitanda na kwenda kwa Mchungaji Mzola wa Kanisa la Hosana Lililopo Nyakasangwa kata ya Wazo kwa ajiri ya kupata huduma ya uponyaji wa kweli.

Na Mwandishi Wetu
Hakika Mungu hutumia watumishi wake kufanya maajabu, hivi ndivyo tunavyoweza kusema. Mchungaji wa Kanisa la Hosana Msigani, Mzola ameendelea kuushanga ulimwengu kutokana na nguvu ya ajabu aliyokuwa nayo ya kuponya watu wenye magonjwa sugu yakiwemo Ukimwi, Kansa nk.
Mchungaji huyo mwenye kanisa dogo tu lililopo Waza mtaa wa Nyakasangwe Msigani lakini amekuwa akifanya mambo ya kushangaza watu kutokana na nguvu ya upako aliyokuwa nayo.
Katika hali isiyokuwa ya kawaida wagonjwa wengi kwa sasa toka Hospitali mbalimbali za Jijini Dar na nje ya Dar wenye magonjwa yaliyoshindikana  wameamua kuacha vitanda na kukimbilia kwa amchungaji huyo tena wakiwa kwenye pikipiki kwa msaada lakini wakanyagapo kwenye ardhi ya kanisa hilo tu, basi hupata uponyaji wa papo kwa hapo.

Hata hivyo mchungaji huyo amewaomba watanzania popote walipo Duniani wasisubiri kifo kiwakute kwa matatizo yanayowasumbua na hata kwa magonjwa sugu kama Ukimwi, Kansa, kichaa, Ugumba, kutokupata mafanikio kwenye biashara  nk wawabebe watu wao na kumlekea ili awape dozi ya Yesu Kristo kwani lisilowezekana kwa binadamu linawezekana kwa Mungu.
Mchugaji aliongeza kusema" Wabebeni wagonjwa wenu na kuwaleta hapa kwenye dozi isiyokuwa na gharama Mungu hashindwi jambo" Alisema na kutoa namba yake ya simu 0713-161785 kwa watu wasioweza kufika kanisani kwake atawapatoa dozi hiyo kwa njia ya simu na watapokea uponyaji huko huko walipo bila gharama yoyote.