TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Monday, January 20, 2014

HUU NDIYO USAFIRI WA MAANA WA LADY JAY DEE, NI GARI YA KISASA ARUSHA DAKIKA SIFURI....!!!


 
Hahaaaa kweli wanaosema wasanii wabongo si wote wenye njaa kama wengi tuzaniavyo, ni juzijuzi tu hapa msanii Diamond Platnumz kavuta mkoko aina ya Toyota Land cruiser V8. Kitendo hicho Diamond kununua gari hiyo kilikua gumzo sana hasa katika mitandao ya jamii ukizingatia gari hilo ni la bei mbaya.
 Sasa mwanadada Lady Jaydee na e kaamua kujibu mapigo kwa kuonyesha mkoko wake mpya aina ya Range Rover Evoque ambayo nayo pia ni ya bei mkasi lakini bado hajamfikia Diamond. Katika tafutatafuta yetu mdakuzi wa XDEEJAYZ alifanikiwa kupata bei za gari hilo kwa nje ya nchi, ambayo kama ni jipya ni kama dola za kimarekani 45,000 ambazo ni sawa na shilingi za ktanzania milioni 72,495.000 na kama limetumika ni kama dola za kimarekani 42,000ambazo ni sawa na 67,662,000.
Kwa msanii kama Lady Jaydee na Diamond kumiliki magari ya ghalama kama hayo ni uthibitisho tosha kua muziki wa Bongo flava unalipa sana kama wasanii wataamua kufanya mziki kama kazi na si masihara. Ni ukweli usiopingika kua wasanii hawa wawili wameweza kua mfano bora kwa jamii kwani mshiko wanaopata wameutumia kuwekeza katika biashara mbalimbali ambazo zimewafanya kuacha kutegemea pato la muziki peke yake.
 
Timu nzima ya xdeejayz inapenda kuwapongeza wasanii hawa kwa mafanikio waliyopata na kwa kuweza kua mfano wa kuigwa na wasanii wachanga ambao nao siku moja wangependa kua kama wao.
"USIKOSE KUSOMA GAZETI LA MASKANI BONGO JUMATANO HII LIKIWA NA HABARI KEMKEM" 

No comments:

Post a Comment