TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Thursday, October 31, 2013

XTREME JEEJAYZ YAWAUNGANISHA WABUNGE WA CHADEMA NA CCMA, WASITISHA KURUDI MAPUMNZIKO KUSUBIRI KUSHUHUDIA LIVE DJ DRUMMER, CLUB MAISHA DODOMA YAWATENGEA SEHEMU MAALUM WAHESIMIWA WOTE!

NI JUMAMOSI YA MSHANGAO NDANI YA CLUB MAISHA NA LIV DJ DRUMMER, ZUNGU MNYAMA AAHIDI KUWAHENYESHWA WAHESHIMIWA WABUNGE NON STOP!


Na Sakina Shabani
Jumamosi ya tarehe 2 mwezi Novemba ni siku ya kukumbukwa kwa wakazi wa mji wa Dodoma na vitongoji vyake kufuatia kufanyika burudani tofauti ambayo haijawahi tokea tangu mkoa huo ambao ni makao makuu ya nchi yetu,
Habari  zilizoshuka kwenye mtandao huu toka kwa meneja Club Maisha Dodoma Dizzo Ismail alisema" Tunaweza kusema kuwa hapa Mkoani Dodoma hakuna stori nyingine zaidi ya mazungumzo yote ni kuhusu Live Dj Drummer itakayofanyika keshokutwa hapa hapa Club Maisha" Alismea  Dizzo
Aidha Dizzo alisema show hiyo imewaunganisha Waheshimiwa Wabunge wa vyama vyote vya upinzani tawala na wadau wote ambapo waheshimiwa hao wanasubiri kushuhudia tukio hilo la vijana wa Xtreme toka Jijini Dar ambao wanaanza kuwasili kesho mkoani hapa kwa ajili ya kufunga mitambo.
Katika hatua nyingine waheshimiwa hao ambao kwa kawaida siku za wikiendi huwa wanarejea makwao baada ya kikao kuwa mapunziko kupisha wikiendi lakini safari hii kwa heshima tu waheshimiwa hao wamegoma kurudi makwao kwa ajili ya kushiriki kwenye burudani hiyo ambayo kimsingi itawaweka akili sawa kabla ya Jumatatu kuendelea na vikao vya bunge.
Dizzo alimaliza kusema wamewaandalia sehemu maalum waheshimwa hao hivyo wanaruhusiwa kuja wote kadri watakavyojaliwa na mwenyezi Mungu kwani licha ya kuwa na mambo mengi ya kufikieia lakini burudani ni sehemu ya kuiongezea akili uwezo kufikiri zaidi. 
Aidha kwa upande wa Dar es salaam meneja msafara huo Hemed Kavu aliiambia blog hii kuwa " Kuna timu mbili ambapo kesho Ijumaa ataanza kuondoka afsa habari mkuu wa Xtreme Deejayz Tanzania Livingstone Mkoi pamoja na mafundi mitambo wa DTV ambapo hao wametangulia kwa ajili ya kuweka sawa mambo madogo madogo, na timu ya pili itaondoka Jumamosi asubuhi mara baada ya kumaliza kutoa burudani huku kwenye Club Maisha Dar" Alisema HK

No comments:

Post a Comment