TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Tuesday, November 26, 2013

TAMASHA KUBWA LA INJILI LA DTV SASA NI DESEMBA 8, WAIMBAJI ZAIDI YA 70 KUUMANA KWENYE JUKWAA MOJA ITAKUWA BALAA!






Na Sakina Shabani
Kituo cha runinga cha Dar es salaam Televisheni DTV kimevunja rekodi kwa kuandaa tamasha kubwa la waimbaji wa nyimbo za Injili linalotarajia kuifanyika mapema mwezi desemba mwaka huu.
Akiongea na gazeti hili mratibu wa tamasha hilo Mathew Philip ambae pia ndiye meneja wa kituo hicho cha maarufu cha runinga alisema “ Ni hivyo tumejipanga kufanya uzinduzi wa kipindi chetu kipya cha SIFA ZA USHINDI kinachorushwa kila siku za Jumapili ndani ya DTV” Alisema meneja huyo
Aidha Meneja huyo aliendelea kueleza kuwa  katika uzinduzi huo wamealikwa wanamuziki zaidi ya sabini toka ndani na nje ya nchi kuja kuhudhuria kwenye uzinduzi huo pamoja na kutoa burudani kwa mashabiki.
Mathew Philip aliongeza kusema kuwa licha ya kwamba tamasha hilo ni la uzinduzi wa kipindi hicho pamoja na uimbaji pia watakuwa na maombo maalum ya kuimbea amani nchi yetu bila kujali itikadi za watu wote. Na wapenzi wa nyimbo za injili wakae mkao wa kula kwani tamasha hilo litakuwa ni la kipekee huenda likawa moja ya matamsha makubwa na yatakayofanya viuzri nchini.
Meneja huyo aliwataja waimbaji hao ambao ni baadhi tu kuwa ni Bahati Bukuk ,Boni Mwaitege, Edson Mwasabwita, Happy kamili, Flora mbasha, Madam Ruti, Neema gasper, Matha Baraka, Siza mwampamba, Prisca Mwalugaja, Elizabeth Nzunda, Davdi Robert, Adelina Swai, Jackline Falles, Sara Mvungi, Victor Aron, Danny Bandezu, Dar gospel, Kwaya ya cvc chang’ombe na wengineo wetu.
Mratibu huyo aliongeza kusema tamasha hilo litafanyika Desemba 8 kwenye viwanja vya Ustawi wa Jamii huku kiingilio kikiwa elfu tano kwa wakubwa na elfu mbili kwa watoto!
"GAZETI LA MASKANI BONGO LITAKUWA MTAANI KUANZIA DESEMBA KAA MKAO WA KULA!!!"

No comments:

Post a Comment