TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Tuesday, January 19, 2016

DC MAKONDA, WAZIRI LUKUVI WASHIKWA PABAYA, TAKUKURU KINONDONI YACHAFUKA, NUSRA WASABABISHE MAUAJI, NI BAADA YA AFISA WAKE ASIYYEKUWA MUADILIFU KUMPIGA VIBAYA MWANANCHI NUSU YA……..!

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar Simon Sirro
 mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Nyakasangwe Peter Bilebela aliyekaa karibu na Mh Paul Makonda ambae anazungumza na wakazi wa eneo hilo.

Huyu ndiye mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Nyakasangwe Peter Bilebela akiwa kwenye moja ya majukumu yake na wananchi hivi karibuni

 Na Mwandisahi wa Maskanibongo gazeti
Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kushtua  hali ya utekelezaji wa agizo la Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni na Waziri wa Ardhi Mheshiwa Lukuvi la kutaka maeneo yote yenye migogoro yapimwe ili kupata ufumbuzi wa mizozo hiyo inayoendelea Jijini , lakini kwa Kata ya Wazo hali imekuwa tofauti baada ya zoezi hilo kuonekana kuwa na dalili zote za kuvurugwa ili likwame.
Habari zaidi zilieleza kuwa  mgogoro huo wa Wazo mtaa wa Nyakasangwe umekuwa na mitihani mingi hasa kwa viongozi wa Serikali ya Mtaa huo unaongozwa na Mwenyekiti wake Peter Bilebela “Mchungaji”  Kwani mgogoro huo unaohusisha watu wenye fedha nyingi ambao hujiita wenye mashamba na wananchi ambao wanaoitwa wavamizi huku nyuma yake kukiwa na masirahi ya baadhi ya vigogo wazito.
Tukio la jana la kukamatwa kwa Mwenyekiti wa Mtaa huo Peter Bilebela na watu waliofika ofisini kwake huku mwenyekiti huyo akiwa kwenye majukumu yake ya kikao na wajumbe huku watu hao wakijitambulisha kama wao ni maafisa TAKUKURU bila kuonesha vitambulisho.
Akiongea kwa masikitiko makubwa Mwenyekiti  mbele ya Kamanda Mkuu  wa TAKUKURU Mkoa wa Kinondoni wakati akihojiwa mara baada ya kufikishwa kwenye Ofisi za Takukuru zilizopo Magomeni Mapipa Jijini Dar es Salaam alisema maafisa hao waliokuwa wametumwa kumkamata walitumia ubabe mkubwa na nguvu nyingi kuliko hekima na ustaarabu kwa kumpiga mbele ya watu.
Mwenyekiti huyo aliendelea kumueleza Mkuu huyo wa Takukuru ambapo Maskanibongo ilifanikiwa kunasa mazungumzo hayo ambapo mwenyekiti huyo alimueleza kamanda huyo kuwa mara baada ya vijana hao kufika ofisini kwake walianza kumkamata mjumbe wake wa Serikali ya mtaa aliyefahamika kwa jina la Mohamed Mangundungundu .
Baada ya kumkata mjumbe huyo aliyekuwa amekaa nje ya ofisi kisha wakamfata Mwenyekiti ambae alikuwa kwenye kikao na kumtaka atoke nje ili apande kwenye gari, lakini mwenyekiti huyo aliwaambia kwamba kuna nini na wao ni akina nani lakini mmoja wa maafisa hao ambae hakufahamika jina lake na ndiye aliyelalamikiwa mwenye matege ya mikono kama baunsa alimjibu mwenyekiti kuwa  yeye hana sababu ya kujitambulisha wala kutoa kitambulisho anatakiwa kupanda gari watafahamiana huko wanakokwenda.
Hali hiyo ilianza kukusanya umati wa watu ambapo kiukweli kitendo cha maafisa hao kutotumia maarifa na akili kutimiza majukumu yao kingeweza kusababisha maafa kwani wananchi wengi walijua ni majambazi wamekuja kumteka mwenyekiti hao hivyo wananchi walishajipanga kwa mapambano na tayari vijan waliashaasha kuchukua silaha za jadi ili kuwakabili watu hao .
Hata hivyo wakati wananchi wakitafakari  juu ya watu hao walikuwa wamegoma kujitambulisha wala kuonesha vitambulisho awari afisa huyo mwenye matege mikononi alimpiga mwenyekiti huyo kibao cha uso hadi miwani kumdondoka huku akimvutia kwenye gari na kufanikiwa kumingiza ndani hapo ndipo walipojitambulisha kama wao ni maafisa wa Takukuru lakini hawakuonesha vitambulisho.
Kabla ya gari hiyo kuondoka wananchi mbali mbali waliokuwa wamefika ofisini pale kupata huduma waliwahoji kwa umakini huku watu maafisa na kuwabana kwa nini wanampiga mwenyekiti huyo ambae alikuwa anabishana nao kimaswali ya msingi ya kutaka wajitambulishe tu basi angeweza kutii, ndipo maafisa hao walipojibu kuwa wao wametumwa kumkamata na kumpiga na mkuu wao ambae ni Kamanda wa TAKUKURU Kinondoni kisha wakawasha gari na kuondoka kwa mwendo wa kasi ya ajabu.
Kimsingi tukio hilo liliwashtua watu wengi ambapo kama si rehema za mungu huwenda lingeweza kuleta maafa kitendo cha maafisa hao kushindwa kutoa vitambulisho mapema na kushindwa kujitambulisha halikuwa jema kwani katika eneo hilo kuna vita inaendelea kati mgogoro wa ardhi kati ya matajiri na wananchi hivyo wananchi wengi walidhani kuwa watu hao ni watekaji kwa jinsi pia walivyokuwa wanatumia ubabe na nguvu nyingi bila hakiri.
Mmoja wa wakazi wa eneo hilo ambae pia ni mtoto wa Waziri Mkuu mstaafu  aliyejitambusha kwa jina la Liberty Msuya alisema “ Ndugu mwandisahi  naweza kusema Mungu kasaidia unauona umati huu watu zaidi ya 800 wamekusanyika nusu saa tu na walikuja hapa kwa baada ya kusikia mwenyekiti wao katekwa na watu wasiofahamika sasa je unadhani wangewakuta hapa nini kingetoa unadhani wangetoka salama wangewezaje kupambana na nguvu hii ya uma? “ Alisema mtoto huyo wa waziri na kushauri kuna haja ya watumishi wa namna hiyo kupewa elimu sahihi jinsi ya kukamata watuhumiwa wao kutoa kitambulisha ni usalama wa kwanza kwao.
Hata hivyo baada ya  wananchi kusikia mwenyekiti wao ameshaondoka umati huo uliekea kituo cha polisi Wazo na kuzajana pale kwa ajiri ya kumuulizia kiongozi wao ambapo maafisa wa ngazi za jauu wa kituo hicho walifanyakazi ya ziada kuwaeleza kama kiongozi wao hayupo na wala hawana taarifa za kukamatwa kwao, licha maafisa wa Polisi kuwauliza kama waliokuja kuwamata walitoa vitambulisho? Lakini ilionekana hawakutoa huku Polisi nao wakiingia hofu huenda mwenyekiti huyo alikuwa ametekwa na wahuni na kuwataka waende kituo cha Polisi Oysterbay.
Viongozi mbalimbali wa Serikali ya Mtaa ambao hawakuwepo eneo la tukio ambapo walimpigia RPC Kinondoni simu na kumueleza tukio hilo ambapo alisema kama watu hao walikuwa wametaja kama wao ni Takukuru  labda waende ofisi zao ndipo walipokwenda na kumkuta akiwa chumbani akihojiwa na maafisa wa ngazi za juu wa Takukuru Kinondoni.
Hata hivyo wananchi mbalimbali wakazi wa kata hiyo ya Wazo wamelani vikali tukio la kudhalilishwa kwa kupigwa mwenyekiti wao mbele ya watu kuhusu suala ya kukamatwa wanasema hawaingilii kwa kama kiongozi wao alikamtwa kwa ajiri ya uchunguzi wa hilo hawapingi kwa vile chombo hicho kina haki na mamlaka ya kufanya hivyo, ila tu kitendo cha kushindwa kuonesha vitambulisho vyao na kumpiga ndicho kimepelekea wao kushikwa na tahamaki kwani awali walijua ametekwa na watu huenda waliokuwa wametumwa na wenye mashamba ili wakamdhuru.
Hali hiyo kiukweli ingeweza kuleta maafa makubwa kwa jinsi staili waliyoitumia kumkamata kibabe mwenyekiti huyo kama kundi lile la watu wangekuwepo  tungeweza kuwakosa maafisa wetu hao wa Takukuru ambao ni muhimu kwa taifa letu hasa kipindi hichi cha kutumbua majibu, hivyo ni heri maafisa hao  baadhi wa Takukuru Kinondoni wakaendelea kupewa elimu au kurudi kwenye mafunzo upya kwa ajiri ya kupata maadili ya kufanya kazi kwa kuzingatia maadili ili kuepuka mdhara kwani hasira waliyokuwa nayo wananchi wa Wazo hakika wangeweza hata kuwachoma moto maafisa hao  kwani wasingeweza kuona mwenyekiti wao akipigwa mbele yao.
Gazeti hili lilifanya jitihada za kumtafuta Kamanda Mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kinondoni ili azungumzie sababu za kumatwa kwa Mwenyekiti huyo ambae alikamatwa akiwa kwenye kikao ofisini  jana tarehe 18 saa kumi jioni na kufikisha makao makuu ya Takukuru ziligonga mwamba mara baada ya simu yake kuita bila kupokelewa hadi habari hii inakwenda mitamboni.
Hata hivyo kitendo cha afisa takukuru huyo kushindwa kutumia akili na maarifa  kwenye utendaji wa kazi yake watu huku akisema katumwa na kamanda mkuu wa Takukuru Mkoa wa Kinondoni ampige mwenyekiti huyo kimetafriwa kama ni kukichafua chombo hicho Mkoa wa Kinondoni kwani haiaminiki kama kweli Kamanda huyo anaweza kumtuma afisa wake ampige mtu asiyekuwa na ubishi, bali itakuwa ni utovu wake wa nidhamu.

No comments:

Post a Comment