TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Monday, November 23, 2015

WATANZANIA WATAKIWA KUMUOMBEA KWA MUNGU PAUL MAKONDA, WAKAZI KINONDONI WAKESHA WAKISALI ILI MUNGU AMFUNGULIE MAMBO YANAYOMSUMBUA ,OFISI YAKE KUTOA TAMKO LEO, MASKANIBONGOTZ INAKUPA FULL STORI..!

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda akiwa ofisni kwake wiki iliyopita alipozungumza na mtandao huu wa habari na matukio wa maskanibongotz, kuhusu utekelezaji wa ahadi yake aliyoitoka miezi 5 iliyopita alipokutana na wakazi wa Nakasangwe na Nakalekwa kuhusu kumaliza mgogoro wa Ardhi kati ya wakazi hao wapatao 2800 wa kata hiyo ya Wazo na mwekezaji mmoja ambae anadai eneo hilo lilikuwa lake licha ya kulitelekeza zaidi ya miaka 25 kwa mujibu wa wazee wa eneo hilo.

Na Mwandishi wa Maskanibongotz

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mh Paul Makonda amevunja rekodi ya kipekee kwa kuanza kutekeleza ahadi aliyoitoa Mh Rais Magufuli kwenye hotuba yake aliyoitoa mwishoni mwa wiki iliyopita  ya kuanza harakati za kuwapimia wananchi ardhi zao na kuwapatia hati miliki zao.
Kauri hiyo pia ikaja kudhihirishwa na Mh Rais ya kuhakikisha wananchi wote wanapimiwa ardhi zao na kupewa hati miliki, wiki hii ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni itatoa ratiba ya kuanza kwa zoezi hilo la kuhakiki viwanja hivyo harafu hatua ya kuimwa ianze kwa kata tatu za Bunje, Madale, na Wazo ambalo maeneo ya Nakasangwe na Nakalekwa ndiye yenye shida sana kutokana na mafisaidi kutumia nguvu ya pesa kuwanyanyasa wakazi hao wanyonge.
Kufuatia hatua hiyo wakazi hao ambao wamesema wana imani na Dc huyo na wanaamini mafisadi hawawezi kumuhonga kama walivyo mtuhumu DC aliyemtangulia Jordan Lugimbana ambae wakazi hao wanadai mafisadi walimshika kisawa sawa na kushindwa kufurukuta kwa nguvu ya pesa.
Hata hivyo wakazi wa Nakasangwe na Nakalekwa toka wiki iliyopita wako kwenye maombi maalum ya kumuomba Mungu amuonngoze vyema Dc huyo kwani ndiye pekee wanaemtegemea kwa sasa kwani katika maafisa wake wa Ardhi nao hawana imani nao kutokana na kuwepo kwenye mkumbo wa rushwa za mafisadi hao .
Wakiongea na maskanibongotz wakazi hao ambao ni watu wazee na vijina wakina mama na wakina baba walisema" Ndugu mwandishi sisi tunaweza kusema kuwa kwa sasa roho na matumaini yetu yako kwa Dc Makonda tu tunamuombea kwa Mungu amuongoze atende haki kwa kusimamia mwenyewe zoezi hili kwani maafisa ardhi wake tulishakosa imani nao siku nyingi kipindi cha Jordan Lugimbana , hivyo watanzania wapenda haki tuungane kumuombea Dc huyo" Walisema wananchi hao.
Kwa kumalizia kumuomba Dc kwenye utekelezaji wa zoezi hilo watu wote wenye vibanda vyao tayari na wanaishi wapewe kipaumbele na hayo maeneo mengine ya ambayo watu hawajajenga ndiyo wapewe hao mafisadi.
Mtandao huu bado unaendelea kumtafuta Dc Makonda ili azungumzie zoezi hilo litaanza tarehe ngapi rasim na wataanza kata gani kati ya hizo zilizotajwa hapo juu, na tutawaleta majibu mapoema iwezekanavyo. 
Credit: Maskanibongotz 


No comments:

Post a Comment