TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Sunday, November 17, 2013

MREMBO HUYU AMTANGAZIA VITA KALI JACKLINE WOLPER, MZEE MAGARI A NAE ATOA ANGALIZO!


 Mrembo/ Msanii wa bongo movie Witness Mmbando akiwa kwenye pozi



Na Sakina Shabani

Mrembo na msanii mpya kwenye kiwanda cha bongo movie aliyefahamika kwa jina la Witness Mmbando “19|” ametoa onyo kali kwa msanii Jackline Wolper  awe makini kwa nafasi anayoishiikilia ya ustaa kwani siku si nyingi atapinduliwa na nafasi yake kuchukuliwa na mrembo huyo mwenye umri mdogo na sifa kibao za kuigiza zaidi ya Wolper.

Habari zilizopatikana mwishoni mwa juma zilisema kuwa Witness ambae ni kabila moja na Jackline Wolper na amekuwa na jazba na Wolper kutokana na msanii huyo kushindwa kuwasaidia wasanii wanaotoka sehemu moja na yeye.

Akiongea na XDEEJAYZ mrembo huyo mwenye elimu ya juu ya Computer alianza kumchana Wolper kwa mambo anayoyafanya huku akisema wasanii wa mkoa wa Kilimanjaro na Arusha jinsi gani wanavyo mchukia “ Unajua Wolper anajisahau sana ameshindwa kuwainua wasanii wachanga wa mkoa wake na kuna wakati mwingine akipigiwa simu anawakatia na kuwajibu vibaya halia ambayo inawakera sana ikizingatia kuwa yeye ndiye mtu wa kuwasaidia kuinua vipaji vyao” Alisema Witness ambae pia ni mtoto wa kigogo wa polisi nchini

Witness aliongeza kusema Wolper alitakiwa hata siku moja kuwatembelea wasanii wa mkoa wake japo kwa kuwapa moyo lakini wapi hata siku moja hajawahi kuitisha hata kikao nao japo kuzungumza nao, hali hiyo imepelea wasanii hao kukosa matumaini na Wolper ambapo anasema sio lazima awapatie pesa la hasha ushauri na maawazo mazuri tu yangetosha.

Mrembo huyo ambae ameonesha kipaji cha hali juu kwenye filamu ya NGEMA ambayo siku za hivi karibuni itakuwa mtaani huku Mzee Magari nae akimtabiria makubwa kwenye ulimwengu wa sanaa kutokana na kipaji chake pamoja na muonekano wake “Huyu binti kwanza umbo lake na uso vinaendana na uigizaji hawa ndio wasanii tunahitaji ili kuzalisha mastaa wengine baada ya sisi kustaafu hivyo Witness namtabiria baraka kwenye tsania hiyo natoa angalizo kwa mastaa wa kike waliopoa sasa kukaa mkao wa kula la sivyo watapotezwa vibaya” Alisema  
KAMA WEWE NI MPENDA BURUDANI HII INAKUHUSU, CLUB MAISHA SASA ZINAPATIKANA DODOMA, MOROGORO,MBEYA,MTWARA NA DAR ES SALAAM HIVYO UKIFANIKIWA KUTEMBELEA KWENYE MOJA YA MIJI HIYO USIKOSE FIKA PALE UJIONEE TOFAUTI YA BURUDANI!

No comments:

Post a Comment