TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Saturday, September 21, 2013

MAELFU YA WATANZANIA WAFURIKA KWENYE MKUTANO WA CHADEMA, MACHUNGU YA MSWADA WA SHERIA NA MAREKEBISHO YAWEKWA HADHARANI!YA


  



Maelfu  wakazi wa jiji la Dar es salaam  wengi wao wakiwa ni  wafuasi wa vyama vya Chadema ,Cuf na NCCR Mageuzi  wemefurika katika  viwanja vya jangwani kuwasilikza  viongozi wakuu wa vyama hivyo ambapo kwa pamoja viongozi hao  wanapinga  hatua  ya serikali  kuingiza baadhi ya vipengele  katika mswada wa  sheria  ya marekebisho  ya  sheria  ya mabadiliko ya katiba .

Viongozi  hao  wanadai  kuwa  vipengele hivyo vitapelekea kupatikana kwa katiba  ya upande mmoja  na kuongeza kuwa kama mswada huo hautafanyiwa marekebisho, basi  wao  hawatashiriki katika bunge la katiba.
  
Katika viwanja hivyo  ulinzi uliimarishwa kutoka katika vikundi mbalimbali  vinavyomilikiwa na vyama hivyo  huku shamra shamra za huko na kule zikiwa hazikosekani ili mradi kunogesha mkutano.   
Mwenyekiti wa taifa wa Chadema  na ambaye  ni kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni Mh Freeman Mbowe amewataka watanzania kuacha uoga na wasimame imara kudai katiba bora.

  Naye mwenyekiti wa Cuf Mh Profesa Ibrahim Lipumba  amesema Tanzani inahitaji katiba ambayo italinda na kusimamia rasilimali za taifa  kuweza kutimia kwa usawa na kuzingatia mahitaji ya watanzania wenyewe.
  Kwa upande wake mwenyekiti wa NCCR Mageuzi  na mbuge wa kuteuliwa amesema hakuna haja ya kutumia  mabavu  na badala yake ameitaka serikali itumie busara zaidi ili kuweza kufikia  mwafaka wa jambo hili

No comments:

Post a Comment