TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Tuesday, November 27, 2012

NILIVYOMJUWA SHARO MILIONEA!


Na Livingstone Mkoi
Kwa kawaida ya binadamu thote tulivyo iwe sehemu yoyote ya kazi kwenye uongozi nk.Huwa tunashindwa kutambua umuhimu wa mtu huyo hadi anapoondoka katika mazingira hayo ndipo umuhimu wake huonekana.
Najaribu kuweka hilo wazi na kimsingi halina ubishi kwani ndio mazoea yetu binadamu na hapa namuelezea kijana mwenzetu ambae ametuacha kwenye ulimwengu huu huku tukiwa tuhahitaji mawazo yake mchango wake nk.
Sharo milionea amefariki kwa sasa huku maelfu ya mashabiki wake wakiwa hawaamini pamoja na mimi mwenyewe kwani mara ya mwisho wiki moja iliyopita nikiwa ofisini kwangu maeneo ya Komakoma EML nilikutana na Sharo na tulizungumza mambo mengi kuhusu gemu ya muziki wa kizazi kipya huku akiniambia kuwa anajiandaa kufanya video ya wimbo wake mpya hivyo atanishtua tushirikiane.
Mimi nilimjibu powa huku tukiachana kwa kupeana mikono lakini wakati naondoka kuelekea Kinondoni Mkwajuni toka Maeneo ya Koma Koma Sharo aliniuliza naelekea wapi ili anape lifti ya gari yake ambapo nilipomjibu ninako elekea aliniambia tuondoke wote na tukaiingia kwenye gari hadi maeneo ya kwangu na kunishusha.

NILIANZA KUMJUWA SHARO TOKA ALIPOIGIZA KOMEDY YA ‘MWEMBWE”
Sharo akiwa chini ya kampuni ya Beknet Production miaka mitano iliyopita huku akiwa na rafiki zake wakubwa Kitale.Kipemba,Kishoka  na wengineo ambapo katika komedy hiyo Sharo alimudu vyema kuigiza hadi kuonekana kuwafunika wenzake hasa kutokana na nafasi aliyokuwa anaigiza pamoja uongeaji mzuri na wa kuvutia  kwa mashabiki wake.
Katika maisha yake Sharo alipenda sana masihara kwa kila mtu na aliheshimu kila mtu pamoja na rafiki zake wakubwa watoto wadogo ambapo hali hiyo ya kujali binadamu wenzake ilimpa umaarufu na kumjengea heshima kubwa nchini.

ANAVYOKUMBUKWA NA MASTAA WENZAKE!
Ni dhahili kuwa kuwa Sharo alikubalika hata na mastaa wenzake hapa MKURUGENZI WA CLUB MAISHA CLAUD CIZA anaelezea namna alivyomjuwa na kumchukulia kama msanii anaetarajia kuja kuwa tishio kimafanikio nchini” Kifo cha Sharo kwa kweli ni kimenigusa sana kama ambavyo kimewagusa wengine nilimjuwa Sharo miaka miwili iliyopita kwa kuangalia kazi zake za sanaa hasa komedy na nikaanza kuwa na ukaribu nae baada ya kuingia kwenye muziki ambapo tulishirikiana mambo mengi sana kwenye muziki” Alisemna Claud

Hata hivyo MKURUGENZI  huyo aliongeza kusema”Sharo alikuwa anatumia juhudi binafsi ili kumletea mafanikio na alikuwa amefanikiwa lakini kwa bahati mbaya ameondoka ghafra na nyota yake kuzimika lakini hata hivyo Mungu apewe utukufu kwa vile yeye ndiye muamuzi wa yote”Alimaza kumuelezea

NISHA MSANII WA BONGO MUVI NAE AMUELEKEZE NAMNA ALIVYOMJUWA SHARO!
Msanii nyota wa bongo muvi Nisha alimuelezea Sharo namna alivyomjuwa”Nilimjuwa Sharo kama kwa mambo mengi kwanza nilimkubari kwenye kazi zake ubunifu kwenye sanaa ulimfanya kila msanii avutiwe nae hivyo sitoweza kumsahau kwa hayo” Alisema Nisha.
MUNGU AMETOA NA AMETWAA JINA LAKE 
LIHIMIDIWE DAIMA AMEN



No comments:

Post a Comment