Msanii nyota kitambo kwenye game ya ugizaji Sintah.
Sintah.
Msanii wa muziki na maigizo nchini Shilole ambae ametangaza kumvulumushia makonde mazito Sintah popote atakapomuona.
Na Livingstone Mkoi
Msanii mkongwe kwenye tasnia ya afrika na kati Sintah amefunguka kuhusu vitisho anavyopewa na msanii mwenzake wa muziki na maigizo Shilole kuwa ajiandae kuchezea kipigo cha mbwa mwizi popote atakapomuona.
Akiongea kwa njia ya simu toka nyumbani kwake Sintah baada ya mtandao huu kutaka kueleza anachukuliaje vitosho hivyo vya Shilole ambapo alisema" Kaka naambiwa sana na watu hasa wanaofatilia mitandao eti natafutwa kupigwa na Shilole sasa ninacho shangaa huyo Shilole anapafahamu kwangu aje basi anipige au kwenye ofisi zangu anapajua namkaribisha vizuri sana jamani" Alisema Sintah
Aidha Sintah aliongeza kusema kuwa" Mimi huwa sio mtu wa maneno yeye aje tu anipige na sio kutangaza kwenye mitandao kuwa ananitafuta anipige hayo mambo ya bifu siku hizi watu wanayachukulia upuuzi kutafuta pesa ndio mpango mzima hivyo mimi namshauri Shilole kama underground wa sanaa nchini aachane na bifu badala yake akazane kwenye mambo yake ya kutafuta pesa kwa ajili ya maisha yake na familia kwani uzee unakuja" Alisema Sintah






















