TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Thursday, May 28, 2015

BALAA KUBWA: BONGO MOVIE WATAKIWA KWENDA KUCHANGIA DAMU MUHIMBILI HARAKA SANA, TEAM LOWASA WAPONGEZWA...!









MWANDISHI WA MASKANIBONGOTZ: 
Wananchi mbalimbali wanaendelea kufika kwa wingi kwenye Hosptali ya Muhimbili kwa ajili ya kusaidia bank ya damu kwa kutoa damu huku wananchi wakiipongeza timu ya Lowasa walienda hivi karibuni kutoa damu zao hali iliyosaidia kwa kiasi kikubwa kuongeza mahitaji ya damu salama. Wakiongea na maskanibongotz wananchi hao wamewaomba wasanii wa bongo movie nao kufanya hivyo kufika Hosptalini hapo kwa ajili ya kutoa damu na sio kuendekeza starehe za kufanya pati na kuendesha magari ya kifahari pamoja na starehe zingine wakati kuna jamii yenye uhitaji ambayo inahitaji msaada wa damu. Hata hivyo wananchi hao waliongeza kusema kuwa wasanii bongo movie ni wengi sana na wanaonekana wanaafya njema hivyo wangehamasisha watu kuchangia damu ili iwe mfano sa kitendo cha kuogopa kwenda kutoa damu kinazusha minong'ono mbalimbali kwenye jamii ikizingatia wao ni kioo cha jamii. Credit: Maskanibongotz 

KAZI IPO MWAKA HUU: MANAIKI SANGA NAE ACHUKUA KADI YA UANACHAMA CHADEMA APANIA KUMNG'OA ANNE MAKINDA KWENYE JIMBO LAKE, TAYARI MAMILIONEA WA KIKINGA WAFANYABIASHARA WAAPA KUMPA SAPOTI MSANII HUYO...!



                                       
  NA MWANDISHI WA MASKANIBONGO MSANII ALIYEWAHI KUKUMBWA NA KASHFA NZITO YA KUPIGA PICHA ZA UCHI ZAIDI ZA WANAWAKE 800 AMBAE ANATOKEA IRINGA AMECHUKUA KADI YA UANACHAMA WA CHAMA CHA CHADEMA NA KUDAIWA YUKO TAYARI KUMNG'OA MBUNGE NA SPIKA ANNE MAKINDA KWENYE JIMBO LAKE. CREDIT: MASKANIBONGOTZ 

HII KALI: WEMA SEPETU NA MAMAAKE WAZUSHA TIMBWILI ZITO BANDARINI WEMA AMCHAPA KOFI POLISI WASWEKWA LUPANGO MASAA 6....!


M Na Mwandishi Wetu Katika hali isiyokuwa ya kawaida staa wa bongo movie Wema Sepetu na Mamaake Miriam Sepetu hivi karibuni walizusha balaa kubwa bandarini huku Wema akidaiwa kumzaba kibao Polisi baada ya kuwazuia kupita sehemu ya VIP. maskanibongtz imetonywa Habari za uhakika zilizonaswa na paparazi wa maskanibongotz zilisema kuwa Wema na Mamaake walifika kwenye bandarini hapo bila kufahamika walipokuwa wanakwenda na baada ya kufika hapo moja kwa moja Wema na Mamaake ambao wote walikuwa wamevaa miwani mieusi na waliingia kwenye geti la watu wanaosafiri kwenda Zanzibar na kwingineko na moja kwa moja waliingia kwenye sehemu ya VIP. Lakini hata hivyo katika hali ya kushangaza Wema na mzazi wake walipita getini na kumchunia Askari aliyekuwepo bila hata kumsalimia hali iliyomfanya afande huyo kuwaita wawili hao ili kurudi kwake lakini Wema akiwa ameshikana mkono na mamaake hawakutii amri hiyo bila shuruti na walimpuuza afande huyo ambae baada aliwafata na kuwazuia ndipo afande huyo alipoishia kula kibao cha haja hadi kushika shavu lake kwa uchungu. Hata hivyo Afande huyo aliamua kukumbushia mazoezi aliyopita Moshi ambapo alichachamaa na kuawarukisha kichurachura wawili hao kisha kuwasweka lupango sehemu moja iliyopo humo humo bandarilini. Kwa mujibu wa chanzo chetu ambacho hakina hata chembe ya shaka kilisema Mama Wema alikuwa anatia huruma kwa mazoezi hayo na kumuomba Afande huyo awahurumie lakini haikusaidia kwani Afande huyo ambae inadaiwa anatoke Mkoa wa Mara alikuwa amepandisha mzuka. Hata hivyo ilidaiwa Wema na Mamaake walikaa kwa masaa 6 ndani toka  saa nane mchana hadi kumi na mbili jioni, mtandao huu wa maskanibongotz ilifanya jitihada za kumtafuta Wema kupitia simu yake ya kiganjani ili kuzungumza nae staa huyo na kuweka bayana madai hayo lakini kwa bahati mbaya simu hiyo haikupatikana licha kupigwa kwa masaa 3. Credit: maskanibongotz 

Monday, May 18, 2015

USTAADH KESI " MTOTO WA MCHUNGAJI" AWAJIA JUU VIONGOZI WANAOUA BINADAMU WENZAO KISA UONGOZI, ASEMA WAGANGA WOTE WANAHUSIKA NA IMANI HIYO WAPIGWE RISASI ILI IWE FUNDISHO ...!

 Ustaadh Kessy na Shekh Sharif Khamis wakipeana miko no baada ya kikao chao na waandishi wa habari hivi karibuni kwa ajili ya utambulisho wa ofisi yao mpya ya Manaklin Natural Heling Clinic iliyopo kwenye msiki wa Kichangani Magomeni Mapipa.
 Ustaadh Kessy akizungumza na wanahabari kuitambulisha ofisi yake  hivi karibuni iliyopo Mburahati ya Tiba Asilia pamoja na kutibu magonjwa sugu ya wakina mama na kupambana na majini wabaya wanaotumiwa na wachawi kuangamiza watu. Hata hivyo Ustaadh Kesi katika mazungumzo hayo aliungana na watanzania pamoja na viongozi wa Serikali kupinga mauaji ya walemavu Albino .
Hata hivyo Shekh huyo alitoa uwito kwa watanzania kufika kwa wingi Clinik kwake hasa wale wanaoteseka na magonjwa ya ajabu ajabu na ambao wako tayari wampigie simu namba 0713-247829 na moja kwa moja watapata huduma hiyo. 
 

Thursday, May 14, 2015

WABURUNDI WAISHIO TANZANIA WAMUOMBA SHEKH SHARIF KHAMIS KUTUA BURUNDI KWA AJILI YA KUWAOMBEA DUA KUEPUSHA MAUAJI YA KUTISHA KWENYE FUJO ZINAZOENDELEA...!






Na Mwandishi Wetu
Wananchi wa Burundi waishio Tanzania wamemuomba kijana Shekh Sharif Khamisi Raia wa Tanzania  ambae kwa sasa yupo nchini Kongo kwa ajili ya huduma ya kuomba dua nchi hiyo kuondokana na vita vya wenyewe kwa wenyewe kutua nchini humo. 
Shekh Sharif Khamis ambae dua zake zimeleta mabadiliko makubwa sana nchini Kongo hivyo kama atatua Burundi atasaidia kuondoa vurugu hizo kwa dua tu na si kutumia nguvu nyingi.

WANANCHI WAIPIGIA SALUT E-FM RADIO KWA KUWA NAO KARIBU KULIKO KITUO KINGINE CHOCHOTE TANZANIA..!