TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Friday, October 31, 2014

MGANGA WA MASTAA NCHINI AZUSHA BALAA KUBWA KWA MASHABIKI WA WEMA SEOETU. ALLY KIBA AHUSISHWA..!


 Mganga wa Mastaa nchini pamoja na Diamond akiwa ofisini kwake.

 Na Sakina Shabani
Yule Mganga aliyejipatia jina kubwa nchini Tanzani baada miti shamba zake kuwasaidia watu wengi sana huku vigogo wa Serikali na mastaa wakimtumia kuwekea sawa mambo yao ya mafanikio amezusha balaa kubwa kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuzungumzia mabalaa yanayomkuta mwanamuziki kipenzi cha watu Diamond
.Kwa mujibu wa mtandao wa mganga huyo ambae miti shamba zake zimepelekwa nchi zilizoathirika na ugonjwa wa Ebola kwa ajili ya majaribio alisema kuwa kuanza kuporomoka kwa mwanamuziki Diamond ni dalili za mwisho wa mwanamuziki huyo kimuziki na tayari nyota yake itachukuliwa na mwanamuziki chipukizi ambae hata hivyo hakumtaja jina.
Baada ya taarifa hizo shemeji zake ambao ni mafans wa Wema walianza kumshambulia mganga huyo ambae kwa sasa yupo Jijini Dar kwa ajili ya kuwahudumia wakazi wa Jiji la Dar huku wengi wakimtukana mganga huyo.
Hata hivyo mganga huyo alipotafutwa na gazeti kupitia namba yake ya simu 0788-8444902 alipatikana na kusema" Unajua Diamond na kijana wangu na tumeshiriki kumuinua lakini kwa hali inavyoonekana tayari mwisho wa ustaa wake umefika na dhahiri shahiri mtu mwingine anakuja kukalia kiti chake" Alisema mganga huyo
Aidha mganga huyo ambae amekuwa akitumiwa sana wafanyabishara pia kusafisha mambo yao kutumia miti shamba zake, huku viongozi wa vyama na siasa nao hawaishi nyumbani kwake kupata baraka zake.
Pia anatibu magonjwa mbalimbali yaliyoshindikana kama uzazi, ganzi miguuni na mikononi, kisukari, Ukimwi kupandisha CD4 kwa wiki moja tu, kumuona mchawi live bila king'amuzi nk. Na ametoa uwito kwa wananchi kuelendelea kuitumia nafasi hiyo kabla hajaondoka msimu huu wa mwisho wa mwaka

WAKATI BONGO MOVIE WAKIOMBOLEZA MSIBA WA MSANII MZEE MANETO, MSANII TINO MADHABU HALI YAKE NI MBAYA ANAHITAJI MSAADA KUNUSURU UHAI WAKE. DUDE ATUHUMIWA KULA HELA ZA MCHANGO..!



MSANII TINO MADHAHABU AMBAE TANGU WIKI ILIYOPITA AMEZIDIWA KWA UGONJWA KUOTA NYAMA PUANI HUKU AKIKOSA MSAADA WA WASANII WENZAKE
 http://www.bongomovies.com/public/uploads/R.I_.P_.jpg
 Wakati mashabiki na wasanii wa Bongo Movie wakiomboleza msiba wa Mzee Manento amefariki dunia hapo juz. kuna taarifa kuwa msanii mwingine wa Bongo Movie Tino Madhahabu nae amelazwa huku akitelekezwa bila msaada huku msanii Dude akituhumiwa kula pesa za mchango wa kumuuguzia msanii huyo.
Kwa mujibu chanzo chetu kiliieleza Maskanibongotz kuwa msanii amekuwa akiugua zaidi ya miaka miliwi na hivi karibuni familia ya msanii huyo  ilitoa taarifa kwenye vyombo vya habari kuhusu kuugua kwa  msanii huyo huku wasanii wenzake kumtelekeza ambapo mtandao huu uliwasiliana na Rais wa Shirikisho la Filamu Tanzania Saimon Mwakifwamba ambae alikuwa amemuagiza Dude afike nyumbani kwa Tino kwa ajili ya kuangalia hali halisi harafu michango ianze kuchangwa kwa ajili ya kunusuru uhai wa msanii huyo.
Hata hivyo kwa mujibu wa Tino mwenyewe alisema kuwa Dude alipiga simu kwake na kumueleza kama amepata taarifa zake toka kwa Rais hivyo ataendesha harambe ya mchango kisha atafika kwake toka hapo hali leo hajawahi kupiga simu kuelezea hiyo harambe imefikia wapi hali inayotia shaka huenda labda amekula mchango huo.
Maskanibongotz ilimtafuta Dude kupitia simu yake ya kiganjani ili kueleza ukweli wa tuhuma hizo ambapo simu ya msanii huyo iliita tu bila kupokelewa.
CREDIT: MASKANIBONGOTZ

BANK YA NMB YAWAKUNA VIJANA DODOMA, MAELFU WAFURIKA KWENYE BONANZA UDOM, WANACHI WACHANGAMKIA FURSA..!


LEO NDIO KILELE CHA BONANZA HILO LILILOANDALIWA NA NMB TAWI LA UDOMA AMBAPO ITAKUWA NDIO FAINALI YA MPIRA WA MIGUU NA  MIKONO SAMBAMBA YA YOTE HAYO PIA KUTAKUWA NA BURUDANI KUTOKA KWA WASANII MBALI MBALI AKIWEMO BARNABA BOY, BONANZA HILO LITAANZA SAA 8 MCHNA NA KUENDELEA NA HAKUNA KIINGILIO


























Wednesday, October 29, 2014

MUZIKI MNENE BAA KWA BAA KUKINUKISHA TEGETA DARAJANI NDANI YA BAA YA KIMORI HIGHWAY PARK. 93.7 E-FM YAZIDI KUTIKISA NCHI WAHESHIMIWA WABUNGE WATOA 5...!


Tarehe 1 Novemba, 2014 ni siku ya kukumbukwa kwa wakazi wa Tegeta Darajani  na vitongoji vyake kufuatia program ya Muziki Mnene baa kwa baa kushusha  bonge la burudani

WALIOMUUA CAPTAIN WA BAFANABAFANA KUTAMBULIWA KITAALAM, MKEWE AELEZEA JINSI WALIVYOMPIGA RISASI HUKU AKIWA NA BUNDUKI YAKE KIUNONI..!

Kelly Kumalo mpenzi wa Senzo akiwa na mtoto wa Senzo Meyiwa.
Polisi nchini Africa Kusini wameonesha nyuso zinazo dhaniwa kuwa ni wauaji wa golikipa na kapteni wa timu ya taifa Africa Kusini Bafana Bafana, Senzo Meyiwa.
Meyiwa alipigwa risasi na kufa siku ya jumapili wakati alipokuwa akikabiliana na wavamizi waloingia nyumbani kwa mpenzi wake Kelly Khumalo ambaye ni mwanamuziki na pia ni muigizaji,maziko ya Meyiwa yanatarajiwa kufanyika mwishoni mwa wiki hii.
Kifo cha mwanasoka huyo kimeonesha picha halisi ya kiwango cha uhalifu na matumizi mabaya ya silaha nchini Africa Kusini.
Africa kusini inatajwa kuwa moja ya nchi zenye matukio makubwa ya uhali,na kiwango cha uhalifu kinazidi kuongezeka siku hadi siku.
Mwanzoni mwa mwezi huu mwanariadha Oscar Pistorious alihukumiwa miaka mitano jela kwa kosa la kumpiga risasi na kumuua mpenzi wake.

ANGALIA ACHOKIZUNGUMZA MBABEJACKIE CHAN BAADA YA MWANAE KUKAMATWA NA MADAWA NCHINI CHINA..!


JackieMkali wa movie kutoka Hong Kong China, Jackie Chan ameomba vyombo vya habari ‘vijichunge’ na namna vinavyoandika taarifa kuhusiana na kitendo cha mtoto wake kukamatwa na dawa za kulevya kwa kuwa kufanya hivyo si kumuumiza yeye (Jackie Chan) bali ni kumuumiza mama wa mtoto huyo.
Jackie Chan amesema kupitia tukio hilo amejifunza kuwa baba bora kitu ambacho hakukijua siku za nyuma.
Mtoto wa staa huyo, Jaycee Chan alikamatwa kwa kosa la kukutwa na dawa za kulevya aina ya bangi zaidi ya gramu 100 ndani ya nyumba yake, na baadaye kushitakiwa kwa kuuza dawa hizo.
Jackie Chan ambaye amekuwa balozi wa kupinga dawa za kulevya tangu mwaka 2009, amesononeshwa na pia ameomba radhi kwa kosa alilotenda mwanae ambapo hii imekuwa mara yake ya kwanza kujibu swali linalohusiana na kesi ya mtoto wake, akisema kupitia hilo amejifunza kuwa baba bora.

BREAKING NEWS: UBUNGO KWA WAKA MOTO HOFU NA MASHAKA KWA WANANCHI WAKIMBIA OVYO KUOKOA MAISHA YAO MUDA HUU...!


 Hii ndiyo hali halisi ya tukio muda huu 
Kamanda wa Polisi Kanda ya Kinondoni Camilius Wambura

Tuesday, October 28, 2014

MISS UTALII AELEZEA JINSI MANAIKI SANG ALIVYOMLAZIMISHA KUMLA "JICHO" NA KUMUHARIBU VIBAYA..!



Mshiriki Miss Utalii Tanzani 2013 pia aliyekuwa balozi wa Hotel zote za Kitalii Tanzania akiwa kwenye picha mahabha nigalgaze.
 Jamaa anaedaiwa kwa sasa kamuoa kabisa Fthiya Kharufan na kumuweka ndani bila kujali yasemwayo.
Hapa pia Fathiya akiwa kwenye picha yake ya Urembo kabla ya kujitoa ufahamu







Na Sakina Shabani
Kha jamani hivyo ndivyo ukiwa kama mzazi unaweza kuonesha mshangao pindi ukisikia maneno haya yanasemwa na mwanao tena kipenzi.
Aliyekuwa mshiriki katika shindano la kumtafuta Miss Utalii Taifa Fathiya Khalfan ameibuka na kutoa tuhuma nzito kwa aliyekuwa mpenzi wake Manaiki Sanga " The Don" Eti kuwa alimlazimisha kumla tendo ambalo kwa sasa limeonekana kushika hatamu kwenye mapenzi ya kileo ambalo limepewa majina lukuki huku wengine wakiita Sauna, Jicho, Kipwinto, mlango wa nyuma, Kiboga na Tigo.
Kwa mujibu wa mtandao wa facebook wa mrembo  huyo alikili kuwa Manaiki Sanga ambae kwa sasa anasema hataki kumuona akiwa hai ama mfu alimsababishia matatizo makubwa katika maisha yake ukiacha suala la picha za uchi lakini jambo jingine zito ni jinsi alivyomfundisha kufanya mapenzi kinyume na maumbile kiasi cha kuzoea hali hiyo.
Fathiya ambae maarufu kama mrembo wa Facebook aliongeza kusema" Namshukuru Maulana huyu mwanaume sio mtu wa kumaindi na kufatilia mambo ya kipuuzi ila nitamuombea Manaiki mabaya hadi naingia kaburini" Alisema Fathiya
Aidha Miss huyo ambae anatoka kwenye familia yenye imani kali huku mwenyewe akisema kuwa Babaake mzazi ni Shekh aliongeza kusema kuwa kwa vile yeye ni msanii na mrembo ameamua kuweka wazi ubaya aliofanyiwa na Manaiki Sanga ambae Fathiya amekili kuwa mmewe wa kupika na kupakua zaidi ya miezi mitano kabla ya kuachana nae.
Maskanibongotz ilifanya jitihada za kumpata Fathiya kupitia simu yake ya kiganjani lakini hakuweza kupatikana lakini alipotafutwa Manaiki alipatikana na kueleza haya" Sasa unataka nikijubu nini kama yeye mwenyewe ameshaongea, ebu acheni mambo yenu ebu andikeni habari za Diamond kukinukisha kwa wanajeshi mmekalia kuandika habari za Manaiki Sanga kwanza picha zenyewe zilipigwa muda sana lakini bado mnafatilia" Alisema Manaiki Sanga
Credit: Maskanibongotz

UKAWA WATIKISA NCHI, MAELFU YA WANANCHI YAWASUBIRI MKOANI KILA KONA HABARI NI MOJA TU JUU YA KUWANG'OA MAFISADI..!



Wabunge wa TZ, ambao baadhi yao wa upinzani wameungana, kuing'oa CCM.

Upinzani nchini Tanzania umetia saini makubaliano ya pamoja, kuking’oa madarakani Chama tawala.
Utiaji huo saini makubaliano ya kukishinda Chama cha Mapinduzi CCM, katika uchaguzi ujao, umefanywa na viongozi wa vyama vinne, huku tukio hilo likishuhudiwa na wafuasi wao.
Katibu Mkuu wa Chama kikuu cha upinzani CHADEMA, Dr. Willibrod Slaa ni miongoni mwa viongozi waliotia saini makubaliano hayo na amesema vyama hivyo vitasimamisha wagombea wake kwa pamoja kwenye ngazi zote za uchaguzi kuanzia serikali za mitaa mpaka ngazi ya urais.
Katibu mkuu wa Chama cha Wananchi CUF, Maalim seif Sharif Hamad anasema tukio hilo la vyama kusaini makubaliano ya kufanya kazi kwa pamoja kwa lengo la kuing’oa CCM ni muhimu na la kihistoria.
Viongozi waliotia saini waraka huo wa makubaliano ni Freeman Mbowe Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani CHADEMA, Profesa Lipumba Mwenyekiti wa Chama cha wananchi CUF, Katibu Mkuu wa Chama hicho ambaye pia ni Makamu wa kwanza rais wa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, James Mbatia Mwenyekiti NCCR Mageuzi, Mosena Nyambabe Katibu Mkuu NCCR Mageuzi, Dr Emmanuel Makaidi Mwenyekiti NLD na Tozzi Matwanga Katibu Mkuu wa NLD.

WANAFUNZI W VYUO WAANZILISHI WA PICHA ZA UTUPU NCHINI TANZANIA, SASA HIVI NI MABOSS WAKUBWA MAOFISINI...!


 Moja ya picha zilizochukua umaarufu nchini na Dunia 
Picha hizi ambazo wahusika hawa walizipiga kwa hiari yao wenyewe na kuzisambaza mitandao kupitia Laptop zao na kusababisha kasheshe la aina yake. ambpo lakini kwa sasa wahusikia hawa ni maboss wakubwa kwenye makampuni mbalimbali. Hata hivyo matokeo mabaya ya wanafunzi kupiga picha za uchi siku za hivi karibuni wameiga picha hizi ambazo wenyewe wamekuwa wakihaha kuziondoa mitandaoni bila mafanikio

VITA MPYA YAIBUKA KATI YA MANAIKI SANGA NA DIAMOND NI BAADA YA MSANII MANAIKI KUMSHAURI DIAMOND KUACHANA NA MUZIKI KWASASA..!


Msanii Manaiki Sanga akiwa na Wema Sepetu ambapo picha hii iliwahi kuzusha balaa kubwa nchini Tanzani kiasi cha kuhatarisha mahusiano ya Wema na Diamond
 

Na Mwandishi Wetu
Mwanamuziki na msanii wa bongo Movie Manaiki Sanga  The Don ametoa ushauri mzito kwa mwanamuziki Naseeb Abdul  a.k.a Diamond na kusema kuwa mwanamuziki huyo anatakiwa kusoma alama za nyakati kipindiu cha ufalme wake kimefika kikomo anatakiwa sasa hivi kuachana na muziki badala yake afanye biashara tu.
Akiongea na mtandao Bossngasa Manaiki Sanga alisema" Napenda kumshauri Diamaond kwa sasa angestaafu kuimba badala yake afanye biashara kwa vile tayari amejikusanyia visenti kidogo na hapo atalinda heshima yake aliyojijengea muda mrefu" Alisema
Hata hivyo msanii huyo aliongeza kusema kuwa kitendo cha kuanza kusomewa hadi Jijini Dar kitafungulia njia hata mikoani au nje ya nchi nako watamzomea au atarushiwa mawe hali itazidi kuwa mbaya zaidi ni heri akaachana na muziki kwa sasa na hii imewakuta wasanii wengi wa Tanzania akiwemo Mr Nice.

NDOA YA MFANYABISHARA MAARUFU KARIAKOO ALIYENASWA MTEGO WA NGONO YASAMBARATIKA..!







 MFANYABIASHARA TAJIRI DAUD MPENDA ALIYENASWA MTEGO WA NGONO
 DUKA LA DAUD MPENDA LA KUUZA SIMU LILIOPO MTAA WA AGREY MWANZO KABISA
Na Sakina Shabani
Unakumbuka lile sakata la mfanyabishara aliyenaswa na kwenye mtego wa ngono baada ta wananchi kuchoka na vitendo vya kifuska hatimae mfanyabishara huyo aliyefahamika kwa jina la Daud Mpenda amerejea nchini siku za hivi karibuni kufuatia kukimbia mji kwa aibu iliyomkuta huku kukiwa na taarifa kuwa mkewe amekimbia nyumba.
Habari za uhakika zilizonaswa na mtandao huu zinasema kuwa tajiri huyo tangu kutokea kwa tukio hilo la kunasa mtego wa ngono baada ya kuwekewa mtego na waandishi wa Habari kufuatia malalamiko mengi ya wananchi juu ya unyanyasaji wanaofanyiwa wasichana wafikapo dukani kwake.
Hata habari hizo zilisema kuwa mke wa Daud ambae ni Mhehe mara baada ya kutokea tukio la kufumaniwa na habari zake zake kusambaa mitandaoni pamoja na kwenye magazeti pendwa  huku picha za ushahidi zikioneka live bila king'amuzi basi mke huyo alifungasha kila kilicho chake na kurudi kwako pia sababu nyingine iliyosababisha kukimbia ni kuhofia maradhi  ya Ugonjwa wa Ukimwi kwani mme huyo ambae hupenda kufanya ngono nzembe.
Daud mbae mara baada ya kufumaniwa ilidaiwa alikimbilia nchini Afrika Kusini kupumnzika  ili so la aibu lipungue..!

Thursday, October 23, 2014

KUNDI LA MAKHIRIKHIRI LA BOTSWANA YAMTEUA MWANDISHI WA E-FM RADIO KUWA MSEMAJI WA KUNDI HILO..!

             



Na Mwandishi Maalum
Kundi la Makhirikhiri la nchini Botswana linaloangozwa na Moses Malapela a.k.a Shumba Latshega limemteua Bwa Livingstone Mkoi msemaji wa kundi hilo nchini Tanzania.
Akiongea na gazeti hili Livingstone Mkoi ambae ni mwandishi wa Habari wa kituo cha E-fm Radio Jijini Dar alisema “ Nilipigiwa simu na Shumba kiongozi wa kundi hilo  ambae ni rafiki yangu mkubwa na kunuieleza kuwa kuanzia sasa nitakuwa msemaji wa kundi hilo hapa nchini Tanzania ambako kundi hilo lina mashabiki wengi sana” Alisema Mkoi
Aidha katika taarifa hiyo Livingstone  aliongeza kusema tayari wameshaingia mkataba wa awali na kiongozi huyo na hivi karibuni mwanamuziki huyo atakuwepo nchini Tanzania kwa ajili ya kuja kuingia mkataba na kampuni LIBE PRODUCTION kwa ajili ya kusambaza albam yake mpya iitwayo  LASO LA MONAMOGOLO mbayo ni moto wa kuotea mbali.
Msemaji huyo aliongeza kusema kuwa katika albam hiyo ambayo baadhi ya nyimbo zake zimefanyiwa nchini Tanzania huku wakielezea usafiri wa bajaj ambao nchini Botswana haupo kabisa na wala hakuna kitu kinachoitwa bajaji.
Kundi la Makhirikhiri liliwahi kuja nchini 2010 na lililetwa na kituo cha Times Radio na kufanikiwa kukonga nyoyo za mshabiki na kuzunguka Tanzania nzima.

Magazeti ya leo October 23 2014 Udaku, Michezo na Hardnews

.
.

.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.
.