TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Tuesday, July 30, 2013

AGNES MASOGANGE APATA TENDA KUCHEZA PICHA ZA X NCHINI AFRIKA KUSINI.VIDEO YAKE YAWAPAGAIWSHA WAZUNGU WAMUANDALIA MAMILIONI YA DOLA MARA ATAKAPOTOA JELA!



HATARIIIIIII MWANAMKE AJIRIPUA NA PETROL PAMOJA NA WANAWE KISA WIVU WA MAPENZI!

SNURA KUACHIA NGOMA MPYA BAADA YA MAJANGA-NIMEVURUGWA

 Yule msanii wa kike aliepewa jina la CAPTEN wa kike wa bongo fleva tanzania,mwenye nyonga isiyonakifani,na mashahiri yatawagusa kila lika hivi karibuni ataachia ngoma yake mpya inayofata baada ya MAJANGA, akiongea na blog hii manager wa msanii huyo hemed kavu HK Alisema wimbo utakuja kuwa ni gumzo la jiji kwamana msanii wangu snura anauwezo wakuimba vitu vingi sana katika nyimbo zake na vyote vina maana na ugusa jamii kwa ujumla, wimbo huu wa NIMEVURUGWA unaelezea watu tofauti walivyovurugwa kwenye MAISHA,SOKA,ELIMU,SERIKALI, na hata kwenye MAPENZI N.K kwa mfano kuna mstari unasema MKANDARASI ALIEPEWA,CEMENT AKAIBA NDIO MANA GHOROFA LIKALETA SHIDA,UZEMBE ULIOFANYWA, WALIMU WAKAGOMA ,WANAFUNZI WAKASHINDWA KUSOMA, NDIO MANA WAKAFELI. Ni nyimbo nzuri sana yenye mashahiri mazito,KAA tayari hivi leo au kesho utasikia.
 
SNURA NA #TEAM MAPACHA

Monday, July 29, 2013

USIKIE USHUHUDA WA KAMANDA WA CHADEMA ALIOUTOA JINSI ALIVYOCHEZEWA NYETI ZAKE NA MWANAMKE MWENZAKE!

KAMANDA WA CHADEMA WANTED.USHUHUDA WAKE WA KUCHEZEWA NYETI NA MWANAMKE MWENZAKE WAMPONZA!


 


Na Mwandishi Wetu
Miezi michache baada  ya  kuvuja  kwa  video  inayomuonesha  mkurugenzi  wa  ulinzi  na  usalama  wa chama  cha  demokrasia  na  maendeleo (CHADEMA),Wilfred Lwakatare  akidaiwa  kupanga  mauaji  ya  mwandishi  wa  habari,video  nyingine  ya  kamanda wa chama  hicho,Linda Bezuidenhout  imenaswa  live....!!
Tofauti  na  video  ya  Lwakatare,hii  ya  Linda inaonesha  mambo  ya  aibu  sana  ambapo  mwanadada  huyo  amerekodiwa  akijieleza  NAMNA  ALIVYO  NUSURIKA  KUSAGWA  NA  MWANAMKE  MWENZAKE.....
Kwa  mujibu  wa  uchunguzi  wetu,Kamanda  huyu  wa  CHADEMA  alirekodiwa  kwa  ridhaa  yake  kwa  lengo  la  kumfikishia  ujumbe  huyo  mwanamke  kwa  uchafu  aliomfanyia....
Katika  video  hiyo, kamanda  huyo  wa  CHADEMA  alijieleza jinsi  alivyokuwa  anasagwa  na mwanamke  huyo....

"Mimi  nimefanya  wema, wema  wangu  umeniponza, wema  wangu  my assssss, wema  wangu  my  fangasi....msenge  we.

"Una wema  wewe?? Ungekuwa  na  wema  ungekuja  kushika  KU**********m  ya  dada  ako  wewe??....mshamba  mkubwa, huna adabu".   Alisema  dada  huyo
Aidha  mwadada  huyo  ambaye  ni  mwanachama  hai  wa  CHADEMA ambaye  amekuwa  akiendesha  harakati  za  chama  hicho  nje  ya  nchi, amemlaumu  dada  huyo   kwa  KUTAKA  KUMSAGA  MPAKA  ALIPKUWA  KATIKA  SIKU  ZAKE  ZA  HEDHI....

Alimlaumu  kwa KUMLAMBA  MIDOMO  YAKE  na  alieleza  kukerwa  siku  mwanamke  huyo   alipokuja  nyumbani  na NYETI  YA  BANDIAA  AKIWA  NA   LENGO  LA  KUMWINGILIA....
Hata  hivyo,Linda  amelaumiwa  vikali  na  watu  walioiona  video  hiyo wakisema  kwamba  alifanya  makosa   kuongea  matusi  makubwa  mbele  ya  watoto  wake.
Mpaka  sasa  haijafahaimka  video  hiyo  imevuja  vipi  na  lengo  hasa  la  kuivujisha.
Aidha uchunguzi uliofanywa na blog hii umebaini kamanda huyo sasa hivi amekuwa wanted na wanawake wenye tabia kama hiyo.Hata hivyo haikufahamika kama wanamtafunia nini?

UKIMWI WAMTESA MSANII BABY MADAHA,ATOA TAMKO ZITO NA LA KUSHANGAZA. MCHUNGAJI AMPA USHAURI WA BURE KUNUSURU MAISHA YAKE!

 

Msanii wa Bongo muvie na muziki Baby Madaha.
 
Na Mwandishi Wetu.
Msanii  wa  filamu  bongo,Baby Madaha  amefunguka  kwamba  siku  akianza  kuona  dalili  za  ugonjwa  wa  UKIMWI  ndani  ya  mwili  wake   atakunywa  sumu  kwa  kuhofia  kuchekwa  na  jamii.
Akiongea  na  mwandishi  wetu,Madaha  amedai  kuwa  kwa  sasa  anaamini  hana  ngoma  maana  siku  zote  hutumia  Kinga (kondom)   ili  asiambikizwe  gonjwa  hilo  japo  hana  uhakika  asilimia  zote  maana  hiyo  ni  mipango  ya  mungu.

"Siukatai  ugonjwa  huo  kwa  kuwa  sijui  ni  lini  naweza  kuupata  hasa  ukizingatia  kwamba  mimi  bado  ni  kijana  mbichi  ambaye  bado  nahitaji  kuifurahia  dunia"...Alisema  Baby Madaha..
Katika  mazungumzo  hayo, Madaha  anadai  kwamba  mpaka  sasa  hakuna  mpenzi  wake  yeyote  aliyekufa  kwa  Ngoma  ingawa  wapo  waliofariki  kwa  maradhi  ya  kawaida  na  ajali....
"Nikijua  tu  nina  ngoma  ni  lazima  ninywe  sumu  ili  kukwepa  balaa  la  wabongo.Najitahidi  kujilinda  ili  nisiudake  mapema"..Alisema Madaha  
Madaha  anadai  kwamba  kitendo  cha  yeye  kujiua  mapema  kitasaidia  kuwaondolea  wasiwasi  wasanii  wenzake  ambao  wataanza  kujiuliza  maswali  mengi  kuhusu  watu  aliowahi  kutoka  nao  kimapenzi
"Nitawasaidia  wasanii  wengine  ambao  nimewahi  changia  nao  mabwana.Najua  wataumia  sana, lakini  ndo  hivyo  tena, hakutakuwa  na  jinsi."Sijasema  nina  UKIMWI,Hapana,nimesema  kwamba  ikitokea  maana  watu  hawakawii  kupindisha  maneno"..Madaha
 
Hata hivyo mchungaji wa Kanisa la kiroho aliyejitambulisha kwa jina la Jemsi Mgundoi amempa ushauri wa bure msanii huyo na kusema" Nimesoma taarifa ya msanii huyo ya kuwa akigundulika ameathirika na UKIMWI atajiua, asifanye hivyo kwani atakuwa amejiongezea dhambi mbele za Mungu wake aliyehai hivyo anachotakiwa kufanya ni kuacha zianaa tu na si vinginevyo" Alisema mtumishi huyo wa bwana

SINTAH AZIDI KUKALIA KUTI KAVU,SKENTO YA KULIWA URODA NA JUMA NATURE YAIBULIWA UPYA MJADALA MZITO WAZUKA KWENYE MITANDAO YA KIJAMII!

\

Msanii Rayuu Alaice
msanii Rayuu alaice
Na Mwandishi Wetu.
Jana, Bongomovies.com imefanya interview kwa njia ya simu na mwanadada msanii Rayuu alaice Bungenzi kuhusiana na mambo mablimbali yanayoandikwa kwenye mitandao na tovuti mbalimbali nchini. 
Katika interview hiyo waliweza kupata mambo manne  kama  ifuatavyo:
1. Hajawai kupiga picha za utupu na kuzisambaza ili kupata umaarufu
Akiongea kwa msisitizo Rayuu amesema kuwa hajawai kupiga picha za utupu na kuzisambaza kwenye mtandao kwa ajili ya kupata umaarufu.

“Sijawai kusambaza picha za utupu ili nipate umaarufu, hizo picha kweli ni zangu na ukizitazama vizuri sio picha za utupu kama watu wanavyosema(?????), ni picha nilizopiga kwenye simu yangu kujiangalia tattoo yangu niliyochora kiunoni lakini kuna marafiki zangu waliochukua simu yangu na sijui ni nani ndio zilisambaa kutokea hapo na kila mtu kuandika stori anayoijua yeye” Alisema.
2. Hafahamiani na wala hajawai kuonana na sintah kwa zaidi ya miaka mingi sana
Rayuu amesema kuwa hajawai kuonana na sintah, wala hafahamiani naye personally na huwa anashangaa sana kwanini mwanadada huyu anamchafua kwenye blog yake.
“Kiukweli mi sifahamiani na Sintah, na wala hatujawahi kuonana kwa kipindi kirefu sana, sasa huwa nashangaa kwanini ananichafua na kunitukana kwenye blog yake. Kuna kipindi nilichoka nikaanza kumjibu lakini baadaye nikaona ni utoto bora ninyamaze kwanza nione kama ataacha lakini nashangaa hakui.
Huyu dada mi huwa simuelewi kwakweli,anagombana na kila mtu, nahisi anaweza kugombana hata na panya. Kwanza ni mtu mzima sana kwangu. 
Nakumbuka mi nimemfahamu yeye wakati teyari kashakuwa maarufu na skendo za uroda kwa Juma nature na mimi nilikuwa bado mdogo sana. Sa sijui kwanini hakui. Kila siku anatukanwa kwenye blog yake lakini wala hajali.”…Alisema Rayuu
3. Marehemu Mzee Kipara ndiye haswa aliyemuingiza kwenye sanaa

Watu wengi hawajui kuwa marehemu mzee kipara ndiye aliyemuingiza Rayuu kwenye sanaa. Rayuu alisema kuwa anakumbuka siku moja kundi la kaole walienda kurekodi igizo  lao mitaa ya nyumbani kwa kina Rayuu na alipowaona alimfuata mzee kipara na kumueleza nia yake na ndipo alipompeleka na kumtambulisha kwenye kundi la kaole na kuanza kupata nafasi ya kuigiza na kufanya mazoezi kundini hapo.
4. Sio mtu wa kutoka sana na akila "bata" anaumwa sana kesho yake
Rayuu amesema yeye sio mtu wa kutoka na kupenda kwenda club kama wengi wanavyodhani bali hupenda sana kushinda ndani kwani akifanya hivyo kesho yake lazima aumwe siku

UKOROFI WASABABISHA MSHIRIKI WA TANZANIA (NANDO ) KUTIMULIWA BIG BROTHER BAADA YA KUGOMBANA NA MSHIRIKI MWENZAKE

 

Jana usiku mara tu baada ya Sulu na Annabel kutolewa kwa kura za watazamaji, Big Brother aliwaita washiriki pamoja katika kikao cha dharura kufuatia ugomvi uliotokea kati ya Nando na Elikem.

Itakumbukwa kwamba siku ya ijumaa ilitokea hali ya kutoelewana kati ya Nando na Elikem. Wawili hawa walitukanana sana na kutishiana mno. Ugomvi huo ulianzishwa na Nando.

Kwa mujibu wa sheria za Big Brother mwaka huu, kuanzisha ugomvi ni kosa ambalo hupelekea kupata 'strike' ama onyo.

3 strike rule ni mtindo unaotumika msimu huu. Kwa mujibu wa Big brother, yeyote atakaye fanya makosa matatu makubwa na kupewa maonyo matatu basi moja kwa moja anatakiwa atimuliwe..

Sheria hiyo imetumika kumtimua Nando kwa sababu 1. Alianzisha ugomvi siku ya Ijumaa, 2. Alishiriki ugomvi na Elikem na 3. Alitishia maisha, "I feel like stabbing him. A nigga like that deserves to die"...

Katika kipindi cha wiki 9 za ushiriki wake katika jumba hilo, Nando amekutwa na misuko suko kadhaa ikiwemo kuwahi kukutwa na kisu katika Party ya Channel O pia kukutwa na mkasi chini ya kitanda kitu ambacho ni kinyume cha sheria za big brother.

Kutokana na ugomvi huo Elikem alipata strike moja.

Big brother alimtaka Nando aondoke katika jumba lake hilo na kutumia fursa hiyo kuwataka washiriki wengine waishi kama watu wazima

Sunday, July 28, 2013

NEW MAISHA CLUB MBEYA HAIJAWAAHI TOKEA, WACHINA WAFANYA VITU ADIMU WASEMA ITAKUWA CLUB BORA AFRICA MASHARIKI NA KATI. MASHABIKI NCHINI ZAMBIA WAISUBIRI KWA HAMU!

 Jengo la New Club Maisha  Dar kama linavyoonekana kwa nje.
 Meneja mkuu wa kampuni ya Entertainment Masters LTD  Kushoto Geoffrey Ndawula. Kampuni hiyo ndio wamiliki wa Club Maisha zote Tanzania
  Hapa ni ramani ya picha ya wachina hao ambao wamesema kwa ndani Club hiyo itakavyoonekana. 
 Sehemu ya kuchezea watu kama inavyoonekana.

 Na Livingstone Mkoi MBEYA.

 Kamapuni inayoongoza kuambukiza virusi vya burudani Tanzania ya Entertainment Masters Limited yenye makao yake makuu Jijini Dar es Salaam imeendelea kutimiza ahadi yake ya kuwafikishia watanzania burudani kila kona ya nchi baada ya kufungua Club mpya Mkoani Mbeya ambayo huenda ikafungulia msimu huu wa sikukuu ya Idd.
Mapapalazi wa Xdeejayz ambao wako kwenye ziara ya kikazi mkoani humo walijionea ujenzi wa Club hiyo mpya  inayosimamiwa na makandarasi toka nchini China na kufanikiwa kuongea na meneja mkuu wa kampuni ya burudani ya Entertainment Masters LTD Geoffrey Ndawula.
Meneja huyo aliiambia Xdeejayz kuwa" Kama tulivyoahidi kuwa azma ya kamapuni yetu ni kuwapelekea watanzania wote burudani huko huko waliko tumenza Mkoani Mtwara kwa mafanikio makubwa na sasa hivi tumetua hapa Mbeya na tutaendelea na mikoa mingine kadri Mungu atakavyotujalia" Alisema Ndawula

Aidha kiongozi huyo aliongeza kusema kwa nini wameajenga Club hiyo mkoani humo." Haya maswali mengi tunaulizwa na mashabiki wetu hasa wa mikoa mingine ambayo huduma yetu haijawafikia, lakini ni dhahili kabisa Mbeya walipaswa kujengewa club ya kisasa kwani wameteseka muda mrefu sana pia tulipokea maombi mengi sana wakihitaji Club Maisha ijengwe hapa hivyo sisi kama bodi ya ungozi wa kampuni yetu tukaamua kufanya hivyo" Alisema meneja huyo.

Hata hivyo ujenzi wa Club Misha hiyo ambao bado unandelea kwa kasi ambapo xdeejayz ilijionea wachina pamoja vibarua wakifanya kazi hiyo kwa kasi kubwa ambapo meneja huyo amesema wanajenga kwa uharaka na huenda sikukuu ya Idd wakaifungua hivyo wanambeya sasa ni zamu yao kula bata hivyo wakae kitako kwa burudani za aina yake

Meneja huyo alishindwa kutoa jengo hilo litatumia thamani ya shilingi ngapi hadi kukamilika licha ya kusema kuwa tayari hadi sasa mamilioni ya shilingi yameshatumika kwenye ujenzi huo.

Friday, July 26, 2013

UGOMVI WA BABA NA MAMA WAUA MTOTO WAO KISHA WAMTUPA KWENYE NYUMBA YA JIRANI ILI KUPOTEZA USHAHIDI, LAKINI JESHI LA POLISI LAWANASA NA KUWATIA NDANI!

 

 

Polisi mkoani Rukwa inawashikilia watu wawili kwa tuhuma za kusababisha kifo cha mtoto wao wakati wanapigana kutokana na wivu wa kimapenzi.

Kamanda wa polisi Mkoa Rukwa, Jacob Mwarwanda amesema tukio hilo lilitokea usiku wa kuamkia Julai 22, saa 5:30 za usiku baada ya Livinus Choma(31) na mkewe  Grace Choma(28) ambao wote wakazi wa Malangali kugombana usiku.

Amesema baada ya mume na mke kurejea nyumbani ulizuka ugomvi baina yao huku mwanamke akimtuhumu mume wake kwamba anauhusiano wa kimapenzi na wanawake wengine na kusababisha waanze kupigana.

Wakiwa wanapigana ghafla mume alimsukuma mke wake ambapo alitereza na kuanguka kitendo kilichosababisha kumlalia mtoto wao aitwaye Esther choma(2)  ambaye alipoteza fahamu hali ambayo wazazi hao walijua wamemuua mtoto wao huyo.

Baada ya mtoto kupoteza fahamu wanandoa hao walichukua mwili wa mtoto huyo na kwenda kuutelekeza katika nyumba ya jirani yao na kisha kupiga simu kwa diwani wa kata hiyo wakidai kuwa mtoto wao amepotea katika mazingira ya kutatanisha.

Diwani huyo alimtaarifu Mwenyekiti wa Serikali ya mtaa na kushirikiana na wazazi hao kuanza kumtafuta mtoto huyo na walimkuta pembeni ya nyumba ya jirani yao akiwa hai, lakini amepoteza fahamu.

Kutokana na hali hiyo walimpeleka katika Hospitali ya Mkoa iliyopo Sumbawanga na kuanza kupatiwa matibabu, lakini alifariki siku iliyofuata kutokana na mauvivu makali aliyoyapata baada ya kuangukiwa na mama yake.

Kutokana na kifo hicho polisi iliwashikila wazazi hao na baada ya kuhojiwa ndipo mama wa mtoto huyo alipoelezea chanzo cha kifo hicho na kudai kuwa walimpeleka mtoto huyo na kumtelekeza kwa jirani ili isijulikane kuwa wao ndiyo waliosababisha kifo hicho na pengine jirani huyo angetuhumiwa kumuiba mtoto huyo na kumuua.

Kamanda Mwarwanda alisema kuwa baada ya upelelezi kukamilika wazazi wa mtoto huyo watafikishwa mahakamani ili wakajibu mashtaka yatakayo wakabiri kufuatia tukio hilo.

MAKAHABA WALIOKAMATWA KIGAMBONI WAMKUMBUKA RAIS OBAMA WA MAREKANI!

 

Friday, July 26, 2013 | 1:33 PM


Awali kachero wa OFM alipokea ujumbe mfupi ulioelezea ufuska unaofanywa na mabinti ambao hupewa eneo na kujenga vibanda kisha kujiuza kwa bei chee katika kijiji hicho maeneo ya Kigamboni jijini Dar.


Mzee Matutu ambaye ni mmiliki wa eneo linalofanyiwa ufuska.
Uchunguzi wa gazeti hili ulibaini kwamba, eneo hilo linalofanyiwa ufuska huo linamilikiwa na kikongwe aliyejitambulisha kwa jina la mzee Matutu akidaiwa kuendesha maisha kwa biashara hiyo ya madanguro.

Baada ya kujiridhisha na uchunguzi kuwa ni kweli jambo hilo linafanyika eneo hilo, OFM ililivamia ikiwa na mjumbe wa mtaa huo aliyefahamika kwa jina la Abbas na kujionea madanguro yaliyojengwa kwa mstari ambapo milango yake iliachwa wazi huku ndani wakionekana mabinti wakiwa wamejilaza kihasarahasara wakiwatega wateja wanaopita katika mtaa huo.
Madanguro hayo ambayo kwa hesabu ni takriban kumi na nane, yamejengwa kwa aina yake ambapo mengi kati ya hayo yana ukubwa wa kutosha kuingia kitanda kidogo pekee.

Baada ya kujionea hayo, kikosi kazi sambamba na mjumbe huyo kilimtafuta mzee Matutu na kufanikiwa kuzungumza naye kuhusu madanguro hayo na namna anavyoyaendesha ambapo alikiri kuwa yeye ni mmiliki wa eneo hilo na huwa anapokea shilingi 30,000 kwa mwezi kwa kila mwanamke na fedha hiyo ndiyo inayomsaidia kuendesha maisha.
Sina kazi nyingine ya kuniingizia kipato zaidi ya hii ya wasichana licha ya kwamba sijawaruhusu wafanye biashara hiyo. Fedha hiyo ndiyo inanisaidia kwa mahitaji yangualisema kwa tabu mzee Matutu huku akimtaja msimamizi wa madanguro hayo kuwa ni mpwa wake.

Kwa upande wake mjumbe wa mtaa huo, Kassim alisema kuwa serikali ya mtaa imejitahidi kwa kadiri ilivyoweza kuwaondoa mabinti hao lakini wamekuwa wakirudi kila mara.
Alipoulizwa hatua waliyoichukua kwa mmiliki wa madanguro hayo ambaye ni mzee Matutu, kiongozi huyo alibakia kusikitika asijue hatua gani ya kumchukulia mzee huyo ambaye hata wakimpeleka kwenye vyombo vya sheria anahisi itakuwa ni uonevu kwa kuwa hana msaada mwingine wa kifedha zaidi ya fedha kutoka kwa mabinti hao.
Makahaba hao waliokamatwa wamesema  wanasikitishwa sana na uonevu unaofanywa na Jeshi la Polisi kuwakamata kamata" Kwa kweli hii sio haki hata kidogo na haikubariki kimataifa kama tungepata nafasi ya kuonana na Rais Obama hakika tungeishtaka Serikali hii na Jeshi lake la Polisi kwa ukatiri wanaotufanyia" Alisema mmoja wa makahaba hao aliyejitambulisha kwa jina la Roza

PADRI ALIYEMTOA NISHAI DADA WA KINGUO CHA UCHI KANISANI ,KULISHITAKI KANISA KWA UDHALILISHAJI ALIOFANYIWA!

 


 Wakati mwanamke wa aliyetolwa nishai mbele ya madhabahu hivi karibuni wakati wa  ndoa  ametishia kulishitaki kanisa hilo kwa kumdhalilisha.
Lakini  Katekista wa Kanisa Katoliki Parokia ya Mtakatifu Peter, Yohane Maboko, amesisitiza kuwa alikiuka maadili ya Kanisa.
Mwanamke huyo ambaye ameendelea kukataa kutaja jina lake, huku njia zingine zikimtaja kwa jina la Restituta Kalemera, alidai juzi kuwa kivazi hicho cha mabega wazi hakikuwa tatizo kanisani, bali ni unyanyasaji tu wa Katekista huyo.
Akizungumza  juzi, alidai kuwa Katekista Maboko alimsukuma na kumwangusha katika ngazi ndefu za Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam.

"Wakati Katekista akinitaka nitoke nje, ghafla alinisukuma nikaanguka kwenye ngazi na kudakwa na mtu mwingine aliyeniokoa, la sivyo ningeumia vibaya," alidai.

Alidai kilichomsikitisha ni kudaiwa kutaka kuingia kanisani akiwa amevaa nguo zilizoacha mwili wazi, jambo ambalo si la kweli, kwa kuwa alikwenda kanisani hapo akiwa na kitambaa kilichofunika mwili.

"Nilipofika kanisani, nilikutana na Katekista akimrudisha mtu mwingine, ghafla alitokea bibi harusi aliyevalia nguo ambazo hazikuruhusiwa kanisani, akaniomba skafu niliyokuwa nayo, nikampa nami kubaki wazi mabegani,"
alidai.

Baada ya kuvua kitambaa hicho, alidai alitaka kuingia kanisani ili kuchukua funguo za gari, lakini alikutana na Katekista kwenye ngazi, ambaye alimwamuru atoke nje naye akaendelea kumsihi kuwa anakwenda kuchukua funguo za gari ndani, hata hivyo hawakukubaliana.

Aliendelea kudai, kuwa Katekista alipomsukuma na kuanguka, baada ya kudakwa alichanganyikiwa akidhani kanisani ni sehemu ya malumbano, akakimbilia ndani kutafakari, huku kiatu chake alichonunua nje ya nchi (Uingereza) kikiwa kimeharibika.

Alidai kuwa akiwa kanisani, Katekista alimfuata tena na kumsihi atoke nje, jambo lililosababisha ndugu zake wamzingire kiongozi huyo wa Kanisa na kumhoji kwa jazba, sababu ya kumsukuma ndugu yao na kuhatarisha maisha yake.

Baada ya malumbano huyo, alitoka nje ya Kanisa na kuacha utaratibu mwingine ukiendelea, huku akilalamika kwamba Kanisa ni sehemu takatifu hivyo hapatakiwi kuwa uwanja wa mapigano na kwamba limeacha kazi ya kufundisha na kuomba ielezwe wazi watu wavae nini.

Akijibu tuhuma hizo, Katekista Maboko alimpongeza mwandishi kwa kushuhudia tukio hilo na kutoa habari yake na kuongeza kuwa utaratibu wa jinsi ya kuingia kanisani kwa maharusi, umekuwa ukifundishwa tangu kuandikishwa kwa ndoa hadi mafundisho ya ndoa.

Alisema dada huyo alipofika kanisani hapo, alikuwa na wanawe wawili waliokuwa na mavazi yaliyoacha sehemu za miili yao wazi, na aliwaelewesha lakini yeye akabisha.

"Niliwashika mikono na kuwapeleka uliko ubao ili wasome maelekezo ya kinachotakiwa kuvaliwa, lakini yeye alilazimisha kuingia huku akisema Mungu haangalii mavazi, bali roho," alisema Katekista Maboko na kuongeza kuwa wakati akieleza hayo, ndipo wanandugu walipofika na kumhoji.

Kuhusu miwani yake kuvunjwa, alisema wakati akiwa amezungukwa na watu kama 30 kwa lengo la kumchanganya, aliendelea kujenga hoja kuwa kanisani zipo taratibu zinazotakiwa kuzingatiwa, lakini mmoja wao alitumia nguvu na kuvunja miwani hiyo.

Hata hivyo, alisema mtu huyo aliomba samahani na kulipa kiasi cha fedha, ambapo walipeana mikono kama ishara ya kusameheana.

Katekista Maboko alisema kwa ufupi kilichotokea, ni kukosekana kwa busara kwa waumini hao, kwani vipo vibao vinavyotoa maelekezo juu ya utaratibu unaotakiwa na unaopaswa kufuatwa.

Thursday, July 25, 2013

MSHIRIKI BBA APIGA PICHA UCHI,ASEMA AMEZIPIGAA MAKUSUDI BAAD YA KUKOSA NAFASI YA KUENDELEA KULA BATA MJENGONI HUMO!

 


Wengi waliamini  kwamba    Big Brother  imempa  fundisho  mrembo  huyu  na  kutegemea  mabadiliko   makubwa  ikiwa  ni  pamoja  na  kuuuheshimu  mwili  wake  baada  ya  Video  zake  za  uchi  kuvuja  akioga  bafuni...
Hali  imekuwa  ni  tofauti  kwa  mrembo  huyu  asiyeijua  thamani  ya  mwili  wake.Tabia  ni  ngozi.Skendo,picha  za  uchi  huenda  ziko  katika  mishipa  ya  damu  yake....
Hizi  ni  picha  zake  za  nusu  uchi  alizotupia  mtandaoni.
 

AIBU NZITO, PADRI WA KANISA AMTOA NISHAI DEMU ALIYEVAMIA HARUSI  YA WATU NA KINGUO CHA UCHI!!!

KIVAZI cha ndugu wa maharusi, kimesababisha patashika katika Kanisa Katoliki, Parokia ya Mtakatifu Peter, baada ya Paroko Msaidizi wa Kanisa hilo, Padri Paulo Haule, kusitisha ibada mpaka mhusika atoke akavae vizuri.
“Ninatoa dakika 10 kwa aliyeingia na mavazi ambayo hayatakiwi kanisani humu kutoka mara moja akavae vizuri, la sivyo ndoa yao haitafungwa,” alisema Padri Haule wa Kanisa hilo lililoko Oysterbay, Dar es Salaam.

Awali vurugu hizo zilizotokea Jumamosi iliyopita, zilianzia nje, wakati Katekista wa Parokia hiyo, Yohane Maboko, alipotangazia wanandoa na ndugu zao waliokuwa mabega wazi au kuvaa nguo fupi, kutafuta nguo za kujifunika au wasiingie kabisa kanisani.
Maharusi walikubali kutekeleza ombi hilo, wakavishwa vitambaa mabegani vya rangi tofauti na gauni jeupe la harusi, wakaruhusiwa kuingia kanisani, tayari kufunga pingu zao za maisha.

Hata hivyo, mmoja wa ndugu wa maharusi hao ambaye jina lake halikupatikana mara moja, alipotaka kulazimisha kuingia na kivazi chake cha mabega wazi, alizuiwa na Katekista Maboko. Katekista huyo alimfuata mwanamke huyo ili kumrudisha akavae vizuri, lakini aliibua zogo na kulazimisha kuingia na vazi hilo.
Zogo hilo lilipoendelea, wanandugu waliingilia kati, wakitetea vazi hilo ambapo mmoja wa wanandugu, alimvua miwani Katekista Maboko na kuipiga chini ikavunjika huku yeye na wenzake wakimtolea maneno makali ya kumtaka asimzuie ndugu yao kuingia kanisani. 
Wakati ndugu hao wakimdhibiti Katekista Maboko, mwanamke huyo alitumia mwanya huo na kupenya hadi ndani ya Kanisa, ambamo Padri Haule, alikuwa akijiandaa kuanza ibada.
Baada ya Padri Haule kupata taarifa, alitangaza kuwa ndoa ya maharusi wa msichana huyo, haitafungwa hadi awe ametoka. 
Licha ya Paroko kutangaza hivyo, bado ukaidi uliendelea jambo lililomfanya Katekista Maboko kumfuata tena dada huyo na kumwamuru atoke nje, ambapo aliendelea kupinga na baadaye akatekeleza amri hiyo ya Paroko.
Baada ya hapo shughuli za kufungisha ndoa ziliendelea kwa amani na utulivu hadi mwisho maharusi wakatoka kwenda kuendelea na mambo mengine.
Akizungumza na mwandishi wetu, Katekista Maboko alisema waumini hao walikiuka maadili ambayo Kanisa lina wajibu wa kulinda na kuyasimamia ili waumini wake wayafuate. 
Alisema miwani yake iliyovunjwa ilikuwa na thamani ya Sh 90,000 na baada ya ibada hiyo, aliyetenda kosa hilo alimwendea na kumwomba radhi na kulipa Sh 50,000 na kuahidi kumalizia kiasi kilichobaki wakati wowote.
Maboko alisema uvaaji wa mavazi yasiyotakiwa kanisani hapo, umekuwa ukipigiwa kelele mara kwa mara, na hata katika mafundisho ya ndoa huambiwa lakini ukaidi unaendelea. 
“Maharusi wakati wa mafundisho ya ndoa tunawaambia kuhusu mavazi yao na hata ya ndugu zao watakaowasindikiza kanisani, kuwa wavae kistaarabu lakini hawasikii,” alisema Katekista Maboko. 
Makanisa mengi siku hizi yamekuwa yakipiga marufuku uvaaji wa nguo fupi na zinazoacha mabega wazi kwa wasichana na wanawake, wakati wa ibada za kawaida na za ndoa.

Tuesday, July 23, 2013

PART II YA PICHA ZA UTUPU ZA MISS UTALII TANZANIA.NUSRA AJIUE KWA SUMU FAMILIA YAKE YAMTENGA,RAIS WA MISS UTALII TZ AMKALIA KOONI HUENDA AKAPOKWA TAJI SIKU YOYOTE!

 Fathiya Khalfani akiwa jukwaani siku ya shindano la kumtafuta mrembo wa taifa "Miss Utalii Taifa" iliyofanyika mwanzoni mwa mwaka huu Mkoani Tanga.




Rais wa Miss Utalii Tanzania Gideon Chipungahelo" Dad"

Na Waandishi Wetu
Hatimae yametimia zile picha chafu zilizonaswa kwa mara ya kwanza na Xdeejayz kisha kusambaa kwenye mitandao mingine sasa zimeonekana kuwa shubiri kufuatia kumtokea puani mrembo Fathiya Khalufan " Mrembo wa Facebook"  kiasi cha kudaiwa kutaka kujiua ili asionekane tena duniani kwa aibu anayoipita.

Baada y wiki moja kupita tangu blog hii kushushiwa cd nzima ya picha za mrembo huyo wa Facebook ambae pia anashikilia taji la ubalozi wa Hotel zote za kitalii Tanzania na kuzirusha kwenye mtandaoni hali imekuwa mbaya kwenye familia ya mrembo huyo.

Habari za uhakika zilizoshuka kwenye ofisi za blog hii toka ndani ya familia hiyo zilisema kuwa Fathiya kwa sasa familia imemtenga kabisa" Jamani muhurumieni ndugu yetu hali ni mbaya hakuna maelewano kabisa kati ya baba mzazi wake pamoja na babaake kwani aibu iliyopo hailezeki msitoe tena kwani mrembo wa facebook mwenyewe amechanganyiwa hajuia la kufanya kanisa" Alisema ndugu huyo aliyeomba hifadhi ya jina lake.

Aidha ndugu huyo aliendelea kusema kuwa" Juzi kati kataka kujiua kwa aibu baada ya familia yake kumsema sana na kumtamkia wazi wazi kuwa itamtenga ndipo alipotishia kunywa sumu lakini hata hivyo dada mkubwa wake alimchukuwa na kumbembeleza" Kilisema chanzo hicho.

Hata hivyo chanzo hicho pia kilisema kuwa tangu kuapia kwa habari hizo Rais wa Miss Utalii Tanzania nae amemkalia kooni mrembo huyo" Chipungahelo nae ambae ndiye boss wake amehitaji maelezo ya msingi kuhusu picha hizo la sivyo atamfungulia mashtaka kisha atanyang'anywa taji hilo" Alisema dada huyo

Mrembo huyo ambae ametamba sana kwenye filamu ya Mrembo wa facebook na huku kwenye mashindano ya Umiss kitaifa akishikilia taji la Ubalozi wa Hotel zote za kitalii Tanzania.

Xdeejayz bado inamsaka kwa udi na uvumba rais wa Miss Utalii Taifa Gedion Chipungahelo "Dad" Ili kuelezea hatua watakazozichukuwa kama wao ungozi ili kukomesha tabia hii mbaya kwa warembo wengine ili heshima ya urembo nchini iweze kuaminiwa na wananchi ambapo kwa sasa wengi wao wamepiga marufuku watoto wao kushiriki mashindano mbalimbali ya umiss kwa madai kuwa ni uhuni kwa matukio kama haya.

MAPYA YAZIDI KUIBUKA KUHUSU MMILIKI WA HOME SHOPPING CENTRE ALIYEMWAGIWA TINDIKALI...!!

 

Tuesday, July 23, 2013 | 11:54 AM

MSHTUKO mkubwa ulijiri Jumamosi iliyopita, ikiwa ni baada ya kusambaa kwa habari za kumwagiwa tindikali, mfanyabiashara mwenye ‘levo’ ya ubilionea, Said Said Mohammed, 42, ambaye ndiye mmiliki na Mkurugenzi Mkuu wa Home Shopping Centre.
 Said ambaye kwa utambulisho mwingine anajulikana kama Said Mohammed Saad, alimwagiwa tindikali Ijumaa iliyopita, saa 2 usiku, lakini habari zake zikavuma Jumamosi, hivyo kuibua taharuki ya aina yake.
Kuhusu nani alimmwagia tindikali hiyo, sababu ya kutendwa unyama huo, yupi mhusika mkuu wa ukatili wenyewe na malengo ya uharamia, kwa jumla, hayo ni maswali yanayoendelea kuitesa familia yake, watu wa karibu pamoja na Jeshi la Polisi Tanzania.
Taarifa za kipolisi zinathibitisha kwamba alimwagiwa tindikali akiwa anazungumza na mfanyakazi wake wa duka lake lililopo kwenye Jengo la Msasani City Mall kisha akakimbizwa Hospitali ya Ami Wellness Centre, iliyopo Masaki, Dar es Salaam kabla ya kupelekwa Afrika Kusini kwa ndege ya kukodi ndani ya kipindi kisichozidi dakika 60.SAID NI NANI?
Ni Mtanzania mwenye asili ya Bara la Asia. Inadaiwa kwamba ndugu zake wengi wana asili ya nchi za Yemen na Saudi Arabia.


Ndiye mmiliki wa Kampuni ya Home Shopping Center. Kampuni hiyo ina maduka mengi Dar es Salaam na katika mikoa kadhaa ambayo yanahusika zaidi na uuzaji wa vitu vya nyumbani na ofisini.
Anatajwa kuwa tajiri mwenye uwezo zaidi katika jumuiya ya wafanyabiashara wa eneo la Kariakoo, kifedha na ushawishi.
Inadaiwa kwamba wafanyabiashara wengi wenye maduka yao Kariakoo, humtegemea yeye kuingiza mizigo nchini, kutokea nje ya nchi hususan China.

Anamiliki nyumba kadhaa za ghorofa Kariakoo, yapo madai kwamba anamiliki nyumba sita.
Baadhi ya majengo ambayo anahusishwa nayo, la kwanza lina ghorofa saba, lipo Mitaa ya Swahili na Msimbazi, la pili lina ghorofa sita, lipo Kongo na Aggrey, tatu ni la ghorofa nne, lipo Barabara ya Uhuru na kadhalika.

Said kupitia kampuni yake ya Home Shopping Centre, aligeuka nyota ya jaha kwa familia 655, zilizokumbwa na mafuriko eneo la Jangwani, Desemba 2011 kisha kuhamishia Mabwepande, Wilaya ya Kinondoni, Dar es Salaam.

Kwa moyo wake mwema, Said aliidhinisha kila familia ipewe seti kamili ya vyombo vya nyumbani pamoja na taa zinazowaka kwa kutumia nishati ya mwanga wa jua.
Misaada hiyo, ilikabidhiwa na mkurugenzi mwingine wa Home Shopping Centre, Ghalib Said Mohammed ambaye ni mdogo wa Said. Misaada hiyo, ilipokelewa na Rais Jakaya Kikwete, Januari mwaka jana.

Said hakuishia hapo, baada ya misaada ya vyombo na taa za nishati ya mwanga wa jua, alifanya jambo jema zaidi kwa kujenga shule ya msingi, madarasa yote pamoja na ofisi za walimu, vilivyojengwa kwa ufadhili wa Home Shopping Centre.
 

Machi mwaka huu, shule hiyo ilizinduliwa na Rais Kikwete ambaye alikiri kwamba ujenzi wake utarahisisha upatikanaji wa huduma za kijamii kwenye eneo hilo.


Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es Salaam, Yusuf Mrefu, alisema kuwa uchunguzi unaendelea kuhusiana na tukio la Said kumwagiwa tindikali Julai 19, mwaka huu.
 

Mrefu alisema, Said alikuwa akizungumza na mfanyakazi wake nje ya duka lake kwenye Jengo la Msasani Mall kisha akatokea kijana mrefu mwembamba ambaye alimmwagia kimiminika kinachosadikiwa kuwa ni tindikali.
 

Kamanda huyo wa polisi aliongeza kwamba mfanyakazi huyo wa Said, Hassan Ahmad, naye alijeruhiwa kidogo katika purukushani hiyo lakini alipopelekwa Hospitali ya Ami Wellness Centre, alitibiwa na kuruhusiwa.

Iadaiwa kuwa Hassan, alipata majeraha baada ya kuanguka, wakati akimfukuza jamaa huyo ambaye alimmwagia tindikali Said.

Mmoja wa wauguzi katika Hospitali ya Ami Wellness, alimwambia mwandishi wetu kwamba baada ya Said kufikishwa pale, ilichukua kama nusu saa, akachukuliwa kupelekwa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere, tayari kwa safari ya kwenda Afrika Kusini.
 

“Hali yake ilikuwa mbaya, lile jicho moja limeathirika sana, kwa kweli sijui kama litaweza kuona tena. Ila moja litakuwa salama, ukizingatia amepelekwa katika hospitali yenye ubora zaidi. Yule mfanyakazi wake aliumia kidogo tu, alitibiwa na kuruhusiwa siku ileile,” alisema muuguzi huyo.
 
Kuhusu jina la hospitali aliyopelekwa, alisema: “Hakukuwa na utaratibu wa kuandika rufaa, alichukuliwa tu kupelekwa Afrika Kusini na sasa naamini anaendelea na matibabu vizuri. Ila inasikitisha sana, naamini wahusika walitaka kumfanya awe kipofu.”

Kwa mujibu wa taswira ya tukio lenyewe, kitendo alichofanyiwa ni umafia na mambo kadhaa yanafaa kumulikwa kwa undani. Mambo hayo ni;
Said ana uadui na nani? Aliyemmwagia alijuaje kama yupo pale? Kwa nini tindikali machoni?
 
Ni wazi Said anao maadui ndiyo maana kitu kile kimetendeka. Bila shaka aliyemmwagia aliambiwa na mtu, huyo anafaa kupatikana. Bila kupindisha ukweli ni kwamba mmwagaji alikusudia kumfanya Said awe kipofu.
 
Polisi wanatakiwa kuchunguza nyendo za Said, kuona ana uhasama na akina nani katika biashara au hata kwenye mambo ya kijamii. Kadhalika, ichunguze mawasiliano ya watu wa karibu na Said, atajulikana mtoa taarifa, hivyo kumpata mhusika wa ukatili pamoja sababu ya unyama wenyewe.

SKENDO ZA SAID
Said ameshawahi kuripotiwa na vyombo vya habari katika kashfa mbalimbali, gazeti moja liliwahi kuandika matoleo kadhaa, likimtaja kama mfanyabiashara hatari kwa nchi ya Tanzania.
 

Vilevile, alishawahi kuripotiwa kumfanyia unyama, kijana mmoja raia wa Lebanon ambaye alidaiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi na dada yake.

FFU WAPINDUKA NA GARI NA MMOJA WAO KUFARIKI PAPO HAPO MKOANI KILIMANJARO..!!

 

Tuesday, July 23, 2013 | 12:26 PM

 
ASKARI mmoja wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) Mkoani Kilimanjaro, Fidelis Mwaliyatabu, amefariki dunia papo hapo na wengine tisa akiwamo Mkuu wa Kikosi hicho kujeruhiwa vibaya baada ya gari lao kupinduka katika kijiji cha Kilingi, wilaya ya Siha, wakati wakienda kuzima vurugu za wananchi.
Ajali hiyo ilitokea wakati kikosi hicho kikielekea katika kijiji cha Karansi kwa ajili ya kukabiliana na wananchi waliokuwa wakiandamana kupinga wenzao waliokamatwa usiku wa manane baada ya kuvamia mashamba mali ya Shirika la Roho Mtakatifu-Kilasara.
Taarifa kutoka kijijini humo zilieleza kwamba wanakijiji waliamua kuandamana baada ya wenzao watano kukamatwa na Jeshi la Polisi nyakati za usiku kwa mahojiano kutokana na kukabiliwa na tuhuma za kushawishi wanakijiji wenzao kuvamia maeneo ya Shule ya Kilasara na kusababisha hasara kubwa kwa shule hiyo.
Kufuatia kukamatwa kwa watuhumiwa hao, wanakijiji waliamua kuaandamana hadi katika kituo cha polisi ili kuwatoa wenzao hali ilisababisha jeshi hilo kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya, jambo ambalo lilishindikana kutokana na wingi wa watu walikuwa wanaandamana.
Inadaiwa kuwa wananchi hao walijikusanya na walianza kuandamana kuanzia majira ya saa 7 usiku kuelekea kituo cha polisi ili kuwatoa wenzao walikuwa wanashikiliwa.
Wananchi wanaoshikiliwa na jeshi hilo ni John Sokoine, Abeli Solomoni, Christopher Solomon na aliyetambuliwa kwa jina moja tu la Julius. Wote walikamatwa usiku wa kuamkia jana.
Mnamo Juni 11, mwaka huu majira ya mchana wananchi wa kijiji hicho walivamia eneo lenye ukubwa wa hekta mbili na kufyeka mazao mbalimbali yaliyokuwa shambani hapo kwa madai kuwa wamiliki wa shule hiyo wamechukua eneo hilo kinyume cha taratibu.
Kwa upande wake, Mkuu wa Shirika la Roho Mtakatifu, Kanda ya Afrika, Padri Jerome Okama, aliushutumu uongozi wa kijiji hicho kwa kuvifumbia macho vitendo vya wananchi kujichukulia sheria mkononi wakati wakitambua kuwa eneo hilo lenye ukubwa wa hekta 8.9 linamilikiwa na shirika hilo kihalali.
Kamanda wa Polisi mkoani hapa, Robert Boaz, akizungumza na NIPASHE kwa njia ya simu kutoka wilayani humo jana jioni, alisema askari hao walipata ajali hiyo majira ya saa 6.45 mchana katika kijiji cha Kilingi nje kidogo ya mji wa Sanya Juu.
Alisema askari hao wamelazwa katika Hospitali ya Rufaa ya KCMC na wengine wamelazwa katika Hospitali ya Taifa ya Ugonjwa wa Kifua Kikuu ya Kibong'oto ilioyopo wilayani Siha na kwamba watano kati yao hali zao ni mbaya.
Alitaja gari la Polisi lililopinduka na kuua kuwa ni Toyota Land Cruiser lenye namba PT 2070 lililokuwa likiendeshwa na Sajenti Herman Dancan. Chanzo cha ajali hiyo ni mwendo kasi na kuacha njia na kupinduka.
Aliwataja waliojeruhiwa katika ajali hiyo kuwa ni Mkuu wa FFU mkoani hapa, ASP Nonino, Renatus Misigalo, Alfonce Joseph, Koplo Elifuraha Lenare, Peter Albert, Bashiri Yusuph, George Mwakyusa na Gaspar Mwapunda.
Alisema mwili wa marehemu umehifadhiwa katika hospitali ya Kibong'oto.

Monday, July 22, 2013

ANGALIA PICHA ZA KANYE WEST ALIVYOPAMABANA NA PAPARAZI ALIYETAKA KUMPIGA PICHA


0719_kanye_west_pap_article

Clash: Kanye West was involved in an altercation with a photographer at LAX on Friday
Clash: Kanye West was involved in an altercation with a photographer at LAX on Friday


Lashing out: The rapper lost his temper at the snapper as he left the terminal
Lashing out: The rapper lost his temper at the snapper as he left the terminal