TANGAZO MAALUM

TANGAZO MAALUM
.

TANGAZA NA SISI

TANGAZA NA SISI KWA BEI NAFUU TUPIGIE KUPITIA 0713 57 57 18 AU TUMA BARUA PEPE DTV@EML.CO.TZ

Friday, November 30, 2012

LEVICIOUS JONSON MWANAMITINDO MWENYE NDOTO YA KUWASAIDIA YATIMA!

 Mwanamitindo nyota nchini Levicious Jonson. 
 Mwanamitindo nyota nchini Levicious Jonson akiwa kwenye moja ya hifadhi za wanyama Mkoani Kilimanjaro.

Mwanamitindo nyota nchini toka Mkoani KilimajaroLevicious Jonson amekuwa na ndoto kuanzisha kituo cha watoto yatima kwa ajili ya kuwasaidia.


Akionge na Xdeejayz mwanamitindo huyo alisema kuwa kila siku amekuwa akisikitishwa na kitendo cha kuwaona watoto wa mtaani wakiteseka bila msaada wowote.

Levicious aliongeza kusema kuwa kwa sasa licha ya kuwa na mipango mingi kuhusu mambo yake ya uanamitindo lakini ameshaweka nadhiri kuwa atakapofanikiwa kimaisha lazima aje kufungua kituo kikubwa cha watoto yatima kwa ajili ya kuwapatia haki za msingi kama elimu.

Mwanamitindo huyo aliongeza kusema"Unajuwa nchi yetu ina watoto wengi sana ambao hawana msaada hivyo nao wanahitaji kusaidia" Alisema mrembo huyo

WATU WALIOMUIBIA SHARO MILIONEA KWENYE AJALI WAKAMATWA KIKOMANDOO!

 Gari ya Marehemu Sharo Milionea kama linavyooneka mara baada ya Ajali iliyopekea kupoteza uhai wake!

Jeshi la Polisi Mkoani Tanga na kushirikiana na wasamalia wema wamewatia mbaroni vijana wanne wanadaiwa kumpora vitu mbalimbali marehemu Sharo Milionea baada ya kupata ajali mbaya mwanzoni mwa wiki hii.

Habari za kuaminika toka Mkoani humo zinasema kuwa vijana hao wamekamatwa baada ya kazi nzuri iliyofanbywa na Jeshi la Polisi Mkoani humo kushirikiana na wasamalia wema ambapo hadi sasa vijana hao wako chini ya ulinzi mkali huku wengine wakiwa bado wanatafutwa.

Habari zaidi zilisema kuwa vijana hao wamekamatwa jana usiku na waliokamatwa wamefahamika kwa jina ya Issa Makunera,Farid Hassani,Rashidi Ayubu,Rashid Makunera na imeelezwa watuhumiwa hao wamekutwa na mali mbalimbali za marehemu.
Chanzo chetu toka mkoani humo zilisema watuhumiwa hao pamoja na mali  hizo zimekamatwa katika eneo linanaloitwa Songa Kibaoni na vitu hivyo ni SPEA TAILI,REDIO YA GARI,BETERI YA GARI,SAA YA MKONONI SURUALI AINA YA JINS PAMOJA TISHETI ,BEGI PAMOJA NA SIMU YA MKONONI.

Hata hivyo habari  ziliendelea kusema kuwa licha ya Begi hilo kupatikana ambalo lilidaiwa ndani yake kulikuwa na pesa nyinge hazikuweza kukutwa na inasemekana katika ya watuhumiwa wanaotafutwa ndio wamekimbia na fedha hizo.

Kufuatia kukamatwa kwa watuhumiwa hao wananchi mbalimbali wamelipongeza  Jeshi la Polisi pamoja na wananchi waeneo waliyokamatwa watuhumiwa kwani wao ndio waliotoa msaada mkubwa hadi kukamatwa kwano.

Aidha Xdeejayz inaendelea kufanya jitihada za kupatikana picha za watuhumiwa pamoja na mali hizo na Soon tutazimwaga kwenye mtandao wetu.

Thursday, November 29, 2012

UKIMWI MPYA WAIBUKA NCHINI HONG KONG,KUTUA NCHINI TANZANIA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA!


WANASAYANSI WASEMA BORA HATA UKIMWI WA ZAMANI ULIKUWA NA NAFUU KULIKO HUU,WAFANYABIASHARA WA KITANZANIA WAHOFIWA KUULETA NCHINI!
Inasemekana mgonjwa huchukuwa wiki moja kuonesha dalili,Mgonjwa huumwa na kukondeana kufa hafi!
Na Mwandishi Wetu kwa msaada wa mitandao

Katika hali isiyokuwa ya kawaida na kushtua kundi la Wanasayansi nchini Hong Kong limegundu ugonjwa mpya ambao unadaiwa kuwa kama ule wa ukimwi unatishia dunia lakini kwa huu ni hatari zaidi ya ukimwi wa kawaida.
Habari zilizothibitishwa na mtandao mmoja nchini humo kupitia taarifa ya jopo la wanasayansi walisema ugonjwa huu mpya ni ukimwi kabisa isipokuwa wenyewe unamuathiri mgonjwa haraka hadi kuugua na akishaanza kuumwa kufa hata kufa lakini mateso makubwa atayaona.
Aidha katika taarifa hiyo iliyothibitsha na Serikali ya nchi hiyo ilisema kuwa ugonjwa huo unatambulika kwa jina la Chyengiruys ambao husababishwa na virusi kama vya ukimwi na baadae mgonjwa huanza kusikia hamu ya kufanya tendo la ndoa zaidi ya mara kumi kwa siku.

Aidha taarifa hiyo iliendelea kueleza kuwa kutokana na maumivu makali yanayotokana na ukiwmi huo mpya watu mbalimbali nchini humo ambao walianza kuugua toka mwaka 2005 walisema kuwa ni bora ukimwi wa zamani una nafuu sana kuliko huu mpya.


SHUHUDIA MAELFU WALIOZIMIA KWENYE MAZISHI YA SHARO MILIONEA


Umati mkubwa ulipelekea mamia wengine kupanda juu ya miti kushudia mazishi ya sharo milionea




Dj Ommy kusho,Ney wa mitego katikati na Dj Makey kulia,walikuepo kwenye mazishi ya sharo milionea










Mamia wazimia baada mwili wa marehemu kuwasiri 






















TUMEJIFUNZA NINI KIFO CHA SHARO MILIONEA?

 Mwanamuziki Mwana FA akisema chochote kupitia DTV  kwenye msiba wa Sharo Milionea.
 Waombolezaji wakiwa wamembeba mwanamke ambae alizimia kwenye msiba wa msanii huyo.
Nape akitoa salamu za rambirambi toka Chama Cha Mapinduzi ccm 
nyumbani kwa Mwanamuziki huyo Mkoani Tanga Jana.


Na  Livingstone Mkoi
Bila shaka kazi ya kumsindikiza kwenye makao ya milele aliyekuwa msanii nyota wa komedi na muziki nchini Sharo Milionea imekwisha lakini sisi tuliobaki tunapashwa kujiuliza tumejifunza nini kutokana na kifo cha ndugu yetu huyu?

Katika maisha ya mwanadamu yana sehemu kuu mbili kuzaliwa na kufa hata hivyo kutokana na usiri wa kutojuwa siku zetu za kufa tatizo ambalo limekuwa likimtatiza kila mmoja.Lakini kubwa zaidi Mungu katupa hali ya kusahau.

Si kama Sharo peke yake bali wengi tumeondokewa na wapendwa wetu kama vile wazazi, watoto wetu na hata wake/Wanaume zetu kila tukifikwa na matukio kama hayo hakika huwa hatuamini kama tutaweza kusahau kamwe lakini kutokana na mipango ya Mungu hali ya kusahau imekuwa ikitufunika sana wanadamu ambapo baada ya kitambo kidogo huwasahau wapendwa wetu waliotutoka.

Hali kadharika kama binadamu tungejuwa siku zetu za kuondoka pengine wengi wetu tungekesha makanisani na misikitini kwa ajili ya kufanya ibada lakini kwa bahati mbaya hakuna afahamue siku yake ya kuondoka duniani zaidi ya Mwenyezi Mungu Muumba Mbingu na vitu vyote vinavyoonekana.

Hata ndugu zetu wazungu.Wanasayansi waliobobea  wamepewa ufahamu na maarifa ya hali ya juu wa kugundua mambo mbalimbali lakini kwa kifo wamegonga mwamba.

Sharo ameondoka na amemaliza kazi yake kwani kiimani ilikuwa ahadi siku yake ya kuondoka ilifika na mapenzi ya Mungu yametimia hilo lazima tukubaliane nalo.Lakini kazi kubwa imebaki kwetu sisi tulio hai je tunajipangaje ili na sisi saa yetu ikifika tuwe tayari tumeweka mazingira sawa ya kukutana na mwenyezi Mungu kwani hakuna imani yoyote ambayo inaruhusu binadamu asifanye mema na atakutana na Mungu!

Kila dini inahimiza binadamu kukumbuka ibada kwa vile ndio njia pekee ya kujiweka karibu na muumba ambapo hata vitabu vyote vinahimiza kukumbuka ibada si vinginevyo.Kwani maisha ya mwanadamu ni mafupi sana ambapo kwa mujibu wa vitabu vyote vya dini kila nafsi lazima itaonja mauti na kila mtu ataondoka kwa wakati wake utakapofika.

Ni ukweli usiopingika Sharo tulimpenda sana na ndio maana wengi wetu turishtushwa sana na taarifa za kifo chake tuliamua kusimamisha shughuri zetu na kusafiri umbali mrefu kwa ajili ya kwenda kushiriki mazishi yake,Kwa kweli Sharo katuachia somo kubwa sana kwetu.

Ukitizama Sharo hakuwa Milionea wa mapesa kama alivyojiita labda usema alikuwa anasaidia watu kuwapatia pesa la hasha bali ni upendo aliokuwa anauonesha kwa binadamu wenzake.
Katika maisha yake Sharo alikuwa rafiki wa kila mtu mtoto mdogo kijana hadi wazee na alipenda sana kushrikiana na watu kwenye matatizo licha ya kwamba hakuna binadamu aliyemakamilifu chini ya jua.

Binadamu tukitambua kuwa maisha yetu ni mafupi sana tunakiwa kuishi kwa upendo mkubwa kwa vile thote ni wapitaji kwenye hii dunia hivyo kutokana na vifo vya wapendwa wetu sio kwa Sharo tu au watu maarufu hapana binadamu wote kwani kwa Mungu hakuna staa, wala tajili thote ni kitu kimoja mbele zake na ndio maana hata tunapokufa huondoka kama tulivyokuja hivyo Upendo ni kitu muhimu sana kwenye maisha yetu ya kila siku.

HISTORIA FUPI YA MAREHEMU HUSSEIN RAMADHANI MKIETI-SHARO MILIONEA


HISTORIA FUPI YA MAREHEMU HUSSEIN RAMADHANI MKIETI-SHARO MILIONEA


Marehemu alizaliwa tarehe 20/03/1987. Marehemu walizaliwa mapacha lakini kwa bahati mbaya pacha mwenzake wa kike alifariki  siku ya pili baada ya kuzaliwa.


Marehemu Hussein ramadhani mkieti alisoma elimu ya msingi katika shule ya msingi ya LUSANGA iliyhopo kijiji cha lusanga wilaya ya MUHEZA na kumaliza mwaka 2001. Marehemu alijiunga na elimu ya secondary mwaka 2002 lakini kwa bahati mbaya kutokana na matatizo ya kifamilia hakuweza kumaliza shule na aliiishia kidato cha pili 2003. Mwaka 2004-2007 alijiunga na shuhuli za ujasiliamali na sanaa mwaka 2008 alijiingiza kwenye maswala ya kuimba na kuigiza comed na filamu, hadi umauti unamkuta HUSSEINI RAMADHANI MKIETI alikuwa ameingia mkataba na kampuny ya E MASTERS  kwa ajili ya kumsimamia kazi zake zote za muziki kwa ukaribu kabisa na HEMED KAVU (HK) ndie alikuwa msimamizi mkuu wa kazi zake. MAREHEMU SHARO MILIONEA AMEZIKWA KWENYE MAKABURI YAKIFAMILIA YALIYOPO KIJIJI CHA LUSAGA MKOANI TANGA KATIKA WILAYA YA MUHEZA.YALIYOPO NYUMA YA NYUMBA YAO.

MAREHEMU HUSEIN MKIETI -( SHARO MILIONEA) HAJAOA WALA HANA MTOTO.

MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU HUSSEIN RAMADHANI MKIETI-SHARO MILIONEA MAHALA PEMA PEPONI AMIN.

Wednesday, November 28, 2012

JIJI LA DAR ES SALAAM LAPOOZA KWA KIFO CHA SHARO MILIONIONE!

 Wananchi wa Jiji la Dar watoto kwa wakubwa wakiwa wamekusanyika barabarani!
Hapa wananchi mbalimbali wakiangalia vichwa vya habari vilivyoandikwa kwenye magazeti mbalimbali kuhusiana na kifo cha mwanamuziki Sharo Milionea.

WANANCHI WENGI WALIOMBA AZIKWE DAR ILI WASHIRIKI MAZIKO YAKE!
.Lakini ilishindikana Watoto wa shule washindwa kujizuia na kujikuta wakiimba nyimbo zake madarasani.
 Na Mwandishi Wetu 
Jiji la Dar es Salaam jana na leo limepooza kufuatia kifo cha aliyekuwa msanii nyota wa muziki wa kizazi kipya nchini Sharo Milionea huku wengi wao wakitamani masanii huyo angezikwa Dar ili nao waweze kushiriki.

Wakiongea na Xdeejayz wakazi hao walisema kuwa kweli kifo hicho kimewasikitisha sana" Kweli tumeumia sana kwa taarifa za msiba huo kwani Sharo alikuwa kipenzi cha watu wote hivyo tumepokea kwa uchungu taarifa hizo" Alisema mkazi wa Magomeni aliyejitambulisha kwa jina la Mama Amina ambae alisema ana mfahamu siku nyingi Sharo
Wananchi waliendelea kusema kuwa kama wangekuwa na uwezo wa kuishawishi familia ya Sharo ili wakubari matakwa yao ni bora wangemzika huku huku Dar ambako ilikuwa maskani yake kubwa.

Kufuatia kifo cha Sharo ambae alizoeleka sana na wa lika zote kutokana na staili yake ya utembeaji,uigizaji,usemaji pamoja na uimbaji hivyo baada ya kifo hicho watoto wengi walishikwa na simanzi ambapo hadi watoto wa shule kushindwa kusoma wakimkumbuka msanii huyo.

"MUNGU AMETOA NA AMETWAA JINA LAKE LIHIMIDIWE DAIWA AMENI"

MAZISHI YA SHARO MILIONEA KUFURU!


 Umati mkubwa wa watu wakiwemo maandishi mbalimbali wa vyombo vya habari wakiwa nyumbani kwao Sharo Milione Mkoani Tanga muda mfupi kabla ya kuelekea Makaburini kwa ajili ya kuupumnzisha mwili wa mwanamuziki huyo.

 Mama Mkubwa wa Sharo ambae hakufahamika jina lake  akilia kwa chungu huku akishindwa kuamini kuhusu kifo cha mwanae huyo

 Kijana aliyedaiwa kuwa mjomba wa Sharo Milionea alishindwa kujizuia kwa simanzi kufuatia kuushuhudia mwili wa Sharo Mochare!

 Rafiki kipenzi wa Sharo Milionea,Kitare akiwa mwenye majonzi makubwa kufuatia kifo hicho.
Muigizaji nyota ambae alikuwa rafiki kipenzi cha marehemu, King Majuto akiel
kea Makaburini kwa ajili ya mazishi ya marehemu Sharo Milionea.


Boti ya abiria ambayo tangu juzi imekuwa ikifanya kazi ya kuwachukuwa waombolezaji toka Kenya hadi Tanga,Ambapo ilidaiwa watu hao ni mashabiki wa mwanamuziki huyo ambae  amezikwa  jioni hii ya leo Mkoani Tanga.
Na Mwandishi Wetu
Mazishi ya aliyekuwa na msanii mahili wa Komedi Tanzania na mwanamuziki wa kizazi kipya Sharo Milionea yameweka historia mpya nchini kufutia umati maelfu ya watu kijitokeza na kumzika.

Habari toka Mkoani Tanga zinasema kazi mbalimbali za kijamii zimesimama leo kwa ajili ya kushiriki kwenye mazishi ya mwanamuziki huyo aliyekuwa kipenzi cha watu nchini ambayo yamefanyika  jioni hii.

Katika hatua nyingie watu toka mikoa mbalimbali tangu jana wamekuwa wakimiminika kwa ajili ya msiba huo ambao umewashtu wengi,waandishi wetu waliopo huko wamesema kuwa msiba huo umehudhuriwa na maelfu ya watu wakiwemo wasanii ambao wameonesha ushirikiano mkubwa  sana kwenye msiba wa msanii mwenzao

Hata hivyo katika hali nyingine Boti za usafiri toka Kenya zimekuwa zikishusha watu zaidi ya mara tatu ambao wote walikuwa wamefika kwa ajili ya kutoa heshima zao za mwisho.
Aidha ndugu wa marehemu wa mwanamuziki huyo waliwapongeza wananchi wote kwa kushiriki pamoja kwenye kipindi hiki kigumu cha kumsindikiza msanii huyo.

Viongozi mbali mbali wa Serikali toka Mkoani humo nao wameshiriki  vyema kwenye mazishi hayo pamoja na kutoa rambirambi zao kwa familia ya marehemu.
MUNGU AILAZE ROHO YA MAREHEMU MAHALI PEMA AMENI

Tuesday, November 27, 2012

NILIVYOMJUWA SHARO MILIONEA!


Na Livingstone Mkoi
Kwa kawaida ya binadamu thote tulivyo iwe sehemu yoyote ya kazi kwenye uongozi nk.Huwa tunashindwa kutambua umuhimu wa mtu huyo hadi anapoondoka katika mazingira hayo ndipo umuhimu wake huonekana.
Najaribu kuweka hilo wazi na kimsingi halina ubishi kwani ndio mazoea yetu binadamu na hapa namuelezea kijana mwenzetu ambae ametuacha kwenye ulimwengu huu huku tukiwa tuhahitaji mawazo yake mchango wake nk.
Sharo milionea amefariki kwa sasa huku maelfu ya mashabiki wake wakiwa hawaamini pamoja na mimi mwenyewe kwani mara ya mwisho wiki moja iliyopita nikiwa ofisini kwangu maeneo ya Komakoma EML nilikutana na Sharo na tulizungumza mambo mengi kuhusu gemu ya muziki wa kizazi kipya huku akiniambia kuwa anajiandaa kufanya video ya wimbo wake mpya hivyo atanishtua tushirikiane.
Mimi nilimjibu powa huku tukiachana kwa kupeana mikono lakini wakati naondoka kuelekea Kinondoni Mkwajuni toka Maeneo ya Koma Koma Sharo aliniuliza naelekea wapi ili anape lifti ya gari yake ambapo nilipomjibu ninako elekea aliniambia tuondoke wote na tukaiingia kwenye gari hadi maeneo ya kwangu na kunishusha.

NILIANZA KUMJUWA SHARO TOKA ALIPOIGIZA KOMEDY YA ‘MWEMBWE”
Sharo akiwa chini ya kampuni ya Beknet Production miaka mitano iliyopita huku akiwa na rafiki zake wakubwa Kitale.Kipemba,Kishoka  na wengineo ambapo katika komedy hiyo Sharo alimudu vyema kuigiza hadi kuonekana kuwafunika wenzake hasa kutokana na nafasi aliyokuwa anaigiza pamoja uongeaji mzuri na wa kuvutia  kwa mashabiki wake.
Katika maisha yake Sharo alipenda sana masihara kwa kila mtu na aliheshimu kila mtu pamoja na rafiki zake wakubwa watoto wadogo ambapo hali hiyo ya kujali binadamu wenzake ilimpa umaarufu na kumjengea heshima kubwa nchini.

ANAVYOKUMBUKWA NA MASTAA WENZAKE!
Ni dhahili kuwa kuwa Sharo alikubalika hata na mastaa wenzake hapa MKURUGENZI WA CLUB MAISHA CLAUD CIZA anaelezea namna alivyomjuwa na kumchukulia kama msanii anaetarajia kuja kuwa tishio kimafanikio nchini” Kifo cha Sharo kwa kweli ni kimenigusa sana kama ambavyo kimewagusa wengine nilimjuwa Sharo miaka miwili iliyopita kwa kuangalia kazi zake za sanaa hasa komedy na nikaanza kuwa na ukaribu nae baada ya kuingia kwenye muziki ambapo tulishirikiana mambo mengi sana kwenye muziki” Alisemna Claud

Hata hivyo MKURUGENZI  huyo aliongeza kusema”Sharo alikuwa anatumia juhudi binafsi ili kumletea mafanikio na alikuwa amefanikiwa lakini kwa bahati mbaya ameondoka ghafra na nyota yake kuzimika lakini hata hivyo Mungu apewe utukufu kwa vile yeye ndiye muamuzi wa yote”Alimaza kumuelezea

NISHA MSANII WA BONGO MUVI NAE AMUELEKEZE NAMNA ALIVYOMJUWA SHARO!
Msanii nyota wa bongo muvi Nisha alimuelezea Sharo namna alivyomjuwa”Nilimjuwa Sharo kama kwa mambo mengi kwanza nilimkubari kwenye kazi zake ubunifu kwenye sanaa ulimfanya kila msanii avutiwe nae hivyo sitoweza kumsahau kwa hayo” Alisema Nisha.
MUNGU AMETOA NA AMETWAA JINA LAKE 
LIHIMIDIWE DAIMA AMEN



SAFARI YA MWISHO YA JOHN S MAGANGA KWENDA KWENYE NYUMBA YAKE YA MILELE


Mwili wa marehemu john s maganga unategemewa kuzikwa leo katika makaburi ya kinondoni kuanzia saa 9 mchana.pichani mwili wa marehemu ukipokelewa kutoka hospital kwa ajili ya sura na mwisho na maziko. r.i.p jonh s maganga.

Monday, November 26, 2012

SHARO MILIONEA AFARIKI DUNIA

 Habari zenye uhakika na zilizothibitishwa ni kwamba sharo milionea amefariki dunia leo hii usiku wa saa 2 kwa ajali ya gari huko MAGUZONI tanga na maiti iko katika hospital ya teule muheza, kwa habari za alieshuhudia ajali kulwa mbondei amesema marehemu alikuwa peke katika  ajali hiyo na alikuwa na gari aina ya HARRIER,Alisema gari iliacha njia na kuingia mapolini na kugonga mti baada ya hapo ilibingirika bingirika zaidi ya mara tatu na kupelekea kifo chake marahemu ameumia sana maeneo ya kichwani na jichoni .hapo ndipo wasamalia wema walipochukua simu yake nakuangalia majina ya watu kwenye simu nakumpigia simu TUNDA MAN kwamba sharo milionea amepata ajali na amefariki maiti ipo hospital ya teule muweza.hapo ndipo taaarifa za kifo cha sharo zilipoanza kusambaa. mungu mlaze mahala pema peponi SHARO MILIONEA













 NA hii ndio chating ya mwisho ya marehemu kabla hajasafiri kwenda tanga


Gari alilopata nalo ajali marehemu HUSSEIN MKIETI a.k.a sharo milionea.